Psalms 49
1Sikieni haya, enyi mataifa yote, 2 sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii. 1
2Wakubwa kwa wadogo, 2 matajiri na maskini pamoja: 1
3Kinywa changu kitasema maneno ya hekima, 2 usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu. 1
4Nitatega sikio langu nisikilize mithali, 2 nitafafanua kitendawili kwa zeze: 1
5Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja, 2 wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka, 1
6wale wanaotegemea mali zao 2 na kujivunia utajiri wao mwingi? 1
7Hakuna mwanadamu awaye yote 2 awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, 2 au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake. 1
8Fidia ya uhai ni gharama kubwa, 2 hakuna malipo yoyote yanayotosha, 1
9ili kwamba aishi milele 2 na asione uharibifu. 1
10Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; 2 wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia 2 na kuwaachia wengine mali zao. 1
11Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, 2 makao yao vizazi vyote; 1 ingawa walikuwa na mashamba 2 na kuyaita kwa majina yao. 1
12Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; 2 anafanana na mnyama aangamiaye. 1
13Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, 2 pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao. 1
14Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, + 49:14 Kaburini hapa ina maana ya Sheol kwa Kiebrania, yaani Kuzimu. 2 nacho kifo kitawala. 1 Wanyofu watawatawala asubuhi, 2 maumbile yao yataozea kaburini, 2 mbali na majumba yao makubwa ya fahari. 1
15Lakini Mungu atakomboa uhai + 49:15 Au: nafsi. wangu na kaburi, 2 hakika atanichukua kwake. 1
16Usitishwe mtu anapotajirika, 2 fahari ya nyumba yake inapoongezeka, 1
17kwa maana hatachukua chochote atakapokufa, 2 fahari yake haitashuka pamoja naye. 1
18Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri, 2 na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa, 1
19atajiunga na kizazi cha baba zake, 2 ambao hawataona kamwe nuru ya uzima. 1
20Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu 2 ni kama wanyama waangamiao.