Psalms 53
1Mpumbavu anasema moyoni mwake, 2 “Hakuna Mungu.” 1 Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa, 2 hakuna hata mmoja atendaye mema. 1
2Mungu anawachungulia wanadamu chini 2 kutoka mbinguni 1 aone kama wako wenye akili, 2 wowote wanaomtafuta Mungu. 1
3Kila mmoja amegeukia mbali, 2 wameharibika wote pamoja, 1 hakuna atendaye mema. 2 Naam, hakuna hata mmoja! 1
4Je, watendao mabaya kamwe hawatajifunza: 2 wale ambao huwala watu wangu 1 kama watu walavyo mkate, 2 hao ambao hawamwiti Mungu? 1
5Hapo waliingiwa na hofu kuu, 2 ambapo hapakuwa cha kutetemesha. 1 Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia; 2 uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau. 1
6Laiti wokovu wa Israeli ungalikuja kutoka Sayuni! 2 Wakati Mungu arejeshapo wafungwa wa watu wake, 2 Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!