Psalms 76
1Katika Yuda, Mungu anajulikana, 2 jina lake ni kuu katika Israeli. 1
2Hema lake liko Salemu, 2 makao yake katika Sayuni. 1
3Huko alivunja mishale imetametayo, 2 ngao na panga, silaha za vita. 1
4Wewe unangʼaa kwa mwanga, 2 mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori. 1
5Mashujaa hulala wametekwa nyara, 2 hulala usingizi wao wa mwisho; 1 hakuna hata mmoja wa watu wa vita 2 anayeweza kuinua mikono yake. 1
6Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, 2 farasi na gari la vita vilikaa kimya. 1
7Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. 2 Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika? 1
8Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, 2 nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya: 1
9wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, 2 kuwaokoa wote walioonewa katika nchi. 1
10Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, 2 na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi. 1
11Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; 2 nchi zote za jirani na walete zawadi 2 kwa Yule astahiliye kuogopwa. 1
12Huvunja roho za watawala; 2 anaogopwa na wafalme wa dunia.