Psalms 24
1Dunia ni mali ya Bwana, na vyote vilivyomo ndani yake, 2 ulimwengu, na wote waishio ndani yake, 1
2maana aliiwekea misingi yake baharini 2 na kuifanya imara juu ya maji. 1
3Nani awezaye kuupanda mlima wa Bwana? 2 Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake? 1
4Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe, 2 yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake 2 au kuapa kwa kitu cha uongo. 1
5Huyo atapokea baraka kutoka kwa Bwana, 2 na hukumu ya haki kutoka kwa Mungu Mwokozi wake. 1
6Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao, 2 wale wautafutao uso wako, Ee Mungu wa Yakobo. 1
7Inueni vichwa vyenu, enyi malango, 2 inukeni enyi milango ya kale, 2 ili mfalme wa utukufu apate kuingia. 1
8Ni nani huyu Mfalme wa utukufu? 2 Ni Bwana aliye na nguvu na uweza, 2 ni Bwana aliye hodari katika vita. 1
9Inueni vichwa vyenu, enyi malango, 2 viinueni juu enyi milango ya kale, 2 ili Mfalme wa utukufu apate kuingia. 1
10Ni nani yeye, huyu Mfalme wa utukufu? 2 Ni Bwana Mwenye Nguvu Zote; 2 yeye ndiye Mfalme wa utukufu.