Psalms 30
1Nitakutukuza wewe, Ee Bwana, 2 kwa kuwa umeniinua kutoka vilindi, 1 na hukuacha adui zangu 2 washangilie juu yangu. 1
2Ee Bwana, Mungu wangu, nilikuita unisaidie 2 na wewe umeniponya. 1
3Ee Bwana, umenitoa Kuzimu, 2 umeniokoa nisishuke kwenye shimo la mauti. 1
4Mwimbieni Bwana, enyi watakatifu wake; 2 lisifuni jina lake takatifu. 1
5Kwa maana hasira yake ni ya muda mfupi, 2 bali upendo wake hudumu siku zote. 1 Inawezekana kilio kiwepo usiku kucha, 2 lakini asubuhi kukawa na furaha. 1
6Nilipofanikiwa nilisema, 2 “Sitatikiswa kamwe.” 1
7Ee Bwana, uliponijalia, 2 uliuimarisha mlima wangu, 1 lakini ulipouficha uso wako 2 nilifadhaika. 1
8Kwako wewe, Ee Bwana, niliita, 2 kwa Bwana niliomba rehema: 1
9“Kuna faida gani katika kuangamia kwangu? 2 Katika kushuka kwangu shimoni? 1 Je, mavumbi yatakusifu? 2 Je, yatatangaza uaminifu wako? 1
10Ee Bwana, unisikie na kunihurumia, 2 Ee Bwana, uwe msaada wangu.” 1
11Uligeuza maombolezo yangu kuwa kucheza, 2 ulinivua nguo za gunia ukanivika shangwe, 1
12ili moyo wangu uweze kukusifu na usikae kimya. 2 Ee Bwana Mungu wangu, nitakushukuru milele.