Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 48

1Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, 2 katika mji wa Mungu wetu, 2 mlima wake mtakatifu. 1

2Ni mzuri katika kuinuka kwake juu sana, 2 furaha ya dunia yote. 1 Kama vilele vya juu sana vya Safoni + 48:2 Safoni inaweza ikawa na maana ya mlima mtakatifu au upande wa kaskazini. ni Mlima Sayuni, 2 mji wa Mfalme Mkuu. 1

3Mungu yuko katika ngome zake; 2 amejionyesha mwenyewe kuwa ngome yake. 1

4Wakati wafalme walipounganisha nguvu, 2 waliposonga mbele pamoja, 1

5walimwona nao wakashangaa, 2 wakakimbia kwa hofu. 1

6Kutetemeka kuliwashika huko, 2 maumivu kama ya mwanamke 2 mwenye utungu wa kuzaa. 1

7Uliwaangamiza kama meli za Tarshishi 2 zilizovunjwa na upepo wa mashariki. 1

8Kama tulivyokuwa tumesikia, 2 ndivyo tulivyoona 1 katika mji wa Bwana Mwenye Nguvu Zote, 2 katika mji wa Mungu wetu: 2 Mungu ataufanya uwe salama milele. 1

9Ee Mungu, hekaluni mwako 2 tunatafakari upendo wako usiokoma. 1

10Ee Mungu, kama jina lako lilivyo, 2 sifa zako zinafika hadi miisho ya dunia, 2 mkono wako wa kuume umejazwa na haki. 1

11Mlima Sayuni unashangilia, 2 vijiji vya Yuda vinafurahi 2 kwa sababu ya hukumu zako. 1

12Tembeeni katika Sayuni, 2 uzungukeni mji, 2 hesabuni minara yake; 1

13yatafakarini vyema maboma yake, 2 angalieni ngome zake, 1 ili mpate kusimulia habari zake 2 kwa kizazi kijacho. 1

14Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; 2 atakuwa kiongozi wetu hata mwisho.

← Psalms 47Read In The App, Free →Psalms 49 →

Study Psalms 48

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150