Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 73

1Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, 2 kwa wale ambao mioyo yao ni safi. 1

2Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; 2 nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama. 1

3Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna 2 nilipoona kufanikiwa kwa waovu. 1

4Wao hawana taabu, + 73:4 Tafsiri nyingine zinasema: hawana maumivu katika kufa kwao. 2 miili yao ina afya na nguvu. 1

5Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, 2 wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine. 1

6Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, 2 wamejivika jeuri. 1

7Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, 2 majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo. 1

8Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, 2 katika majivuno yao wanatishia kutesa. 1

9Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, 2 nazo ndimi zao humiliki duniani. 1

10Kwa hiyo watu wao huwageukia 2 na kunywa maji tele. + 73:10 Au: na kupokea yote wasemayo. 1

11Wanasema, “Mungu awezaje kujua? 2 Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?” 1

12Hivi ndivyo walivyo waovu: 2 siku zote hawajali, 2 wanaongezeka katika utajiri. 1

13Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, 2 ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia. 1

14Mchana kutwa nimetaabika, 2 nimeadhibiwa kila asubuhi. 1

15Kama ningesema, “Nitasema hivi,” 2 ningelikuwa nimewasaliti watoto wako. 1

16Nilipojaribu kuelewa haya yote, 2 yalikuwa magumu kwangu kuelewa. 1

17Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, 2 ndipo nilipotambua mwisho wao. 1

18Hakika unawaweka mahali pa utelezi, 2 unawaangusha chini kwa uharibifu. 1

19Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, 2 wanatoweshwa kabisa na vitisho! 1

20Kama ndoto mtu aamkapo, 2 hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, 2 utawatowesha kama ndoto. 1

21Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, 2 na roho yangu ilipotiwa uchungu, 1

22nilikuwa mpumbavu na mjinga, 2 nilikuwa mnyama mkatili mbele yako. 1

23Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, 2 umenishika mkono wangu wa kuume. 1

24Unaniongoza kwa shauri lako, 2 hatimaye utaniingiza katika utukufu. 1

25Nani niliye naye mbinguni ila wewe? 2 Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe. 1

26Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, 2 bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu 2 na fungu langu milele. 1

27Wale walio mbali nawe wataangamia, 2 unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako. 1

28Lakini kwangu mimi, 2 ni vyema kuwa karibu na Mungu. 1 Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; 2 nami nitayasimulia matendo yako yote.

← Psalms 72Read In The App, Free →Psalms 74 →

Study Psalms 73

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150