Psalms 90
1Bwana, wewe umekuwa makao yetu 2 katika vizazi vyote. 1
2Kabla ya kuzaliwa milima 2 au hujaumba dunia na ulimwengu, 2 wewe ni Mungu tangu milele hata milele. 1
3Huwarudisha watu mavumbini, 2 ukisema, “Rudini mavumbini, enyi wanadamu.” 1
4Kwa maana kwako miaka elfu 2 ni kama siku moja iliyokwisha pita, 2 au kama kesha la usiku. 1
5Unawatowesha wanadamu katika usingizi wa kifo, 2 nao ni kama majani machanga ya asubuhi: 1
6ingawa asubuhi yanachipua, 2 ifikapo jioni huwa yamenyauka na kukauka. 1
7Tumeangamizwa kwa hasira yako 2 na tumetishwa kwa ghadhabu yako. 1
8Umeyaweka maovu yetu mbele yako, 2 dhambi zetu za siri katika nuru ya uwepo wako. 1
9Tumeishi siku zetu zote chini ya ghadhabu yako, 2 tunamaliza miaka yetu kwa kuomboleza. 1
10Siku zetu za kuishi ni miaka sabini, 2 au miaka themanini ikiwa tuna nguvu, 2 lakini yote ni ya shida na taabu, 2 nazo zapita haraka, nasi twatoweka. 1
11Ni nani ajuaye nguvu za hasira yako? 2 Kwa maana ghadhabu yako ni kubwa 2 kama hofu tunayopaswa kuwa nayo kwako. 1
12Tufundishe kuzihesabu siku zetu vizuri, 2 ili tujipatie moyo wa hekima. 1
13Ee Bwana, uwe na huruma! Utakawia hata lini? 2 Wahurumie watumishi wako. 1
14Tushibishe asubuhi kwa upendo wako usiokoma, 2 ili tuweze kuimba kwa shangwe na kufurahi siku zetu zote. 1
15Utufurahishe kulingana na siku ulizotuadhibu, 2 kulingana na miaka tuliyotaabika. 1
16Matendo yako na yaonekane kwa watumishi wako, 2 utukufu wako kwa watoto wao. 1
17Wema wa Bwana Mungu wetu uwe juu yetu; 2 uzithibitishe kazi za mikono yetu: 2 naam, uzithibitishe kazi za mikono yetu.