Psalms 104
1Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. 1 Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, 2 umejivika utukufu na enzi. 1
2Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, 2 amezitandaza mbingu kama hema 1
3na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. 1 Huyafanya mawingu kuwa gari lake, 2 na hupanda kwenye mbawa za upepo. 1
4Huzifanya pepo kuwa wajumbe + 104:4 Au: malaika. wake, 2 miali ya moto watumishi wake. 1
5Ameiweka dunia kwenye misingi yake, 2 haiwezi kamwe kuondoshwa. 1
6Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, 2 maji yalisimama juu ya milima. 1
7Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, 2 kwa sauti ya radi yako yakatoroka, 1
8yakapanda milima, yakateremka mabondeni, 2 hadi mahali pale ulipoyakusudia. 1
9Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, 2 kamwe hayataifunika dunia tena. 1
10Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, 2 hutiririka kati ya milima. 1
11Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, 2 punda-mwitu huzima kiu yao. 1
12Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, 2 huimba katikati ya matawi. 1
13Huinyeshea milima kutoka orofa zake, 2 dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake. 1
14Huyafanya majani ya mifugo yaote, 2 na mimea kwa watu kulima, 2 wajipatie chakula kutoka ardhini: 1
15divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, 2 mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, 2 na mkate wa kutia mwili nguvu. 1
16Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, 2 mierezi ya Lebanoni aliyoipanda. 1
17Humo ndege hufanya viota vyao, 2 korongo ana nyumba yake kwenye msunobari. 1
18Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, 2 majabali ni kimbilio la pelele. 1
19Mwezi hugawanya majira, 2 na jua hutambua wakati wake wa kutua. 1
20Unaleta giza, kunakuwa usiku, 2 wanyama wote wa mwituni huzurura. 1
21Simba hunguruma kwa mawindo yao, 2 na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu. 1
22Jua huchomoza, nao huondoka, 2 hurudi na kulala katika mapango yao. 1
23Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, 2 katika kazi yake mpaka jioni. 1
24Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! 2 Kwa hekima ulizifanya zote, 2 dunia imejaa viumbe vyako. 1
25Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, 2 imejaa viumbe visivyo na idadi, 2 vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo. 1
26Huko meli huenda na kurudi, 2 pia Lewiathani, + 104:26 Lewiathani ni mnyama mkubwa wa baharini mwenye magamba anayefanana na joka kubwa, mwenye umbo la kutisha, asiyeweza kuvuliwa. uliyemuumba acheze ndani yake. 1
27Hawa wote wanakutazamia wewe, 2 uwape chakula chao kwa wakati wake. 1
28Wakati unapowapa, 2 wanakikusanya, 1 unapofumbua mkono wako, 2 wao wanashibishwa mema. 1
29Unapoficha uso wako, 2 wanapata hofu, 1 unapoondoa pumzi yao, 2 wanakufa na kurudi mavumbini. 1
30Unapopeleka Roho wako, 2 wanaumbwa, 2 nawe huufanya upya uso wa dunia. 1
31Utukufu wa Bwana na udumu milele, 2 Bwana na azifurahie kazi zake: 1
32yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, 2 aigusaye milima, nayo ikatoa moshi. 1
33Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; 2 nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi. 1
34Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, 2 ninapofurahi katika Bwana. 1
35Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia 2 na waovu wasiwepo tena. 1 Ee nafsi yangu, msifu Bwana. 1 Msifuni Bwana. + 104:35 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah.