Psalms 101
1Nitaimba juu ya upendo wako na haki yako; 2 kwako wewe, Ee Bwana, nitaimba sifa. 1
2Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama: 2 utakuja kwangu lini? 1 Nitatembea nyumbani mwangu 2 kwa moyo usio na lawama. 1
3Sitaweka mbele ya macho yangu 2 kitu kiovu. 1 Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani; 2 hawatashikamana nami. 1
4Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami; 2 nitajitenga na kila ubaya. 1
5Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri, 2 huyo nitamnyamazisha; 1 mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi 2 huyo sitamvumilia. 1
6Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi, 2 ili waweze kuishi pamoja nami; 1 yeye ambaye moyo wake hauna lawama 2 atanitumikia. 1
7Mdanganyifu hatakaa 2 nyumbani mwangu, 1 yeye asemaye kwa uongo 2 hatasimama mbele yangu. 1
8Kila asubuhi nitawanyamazisha 2 waovu wote katika nchi; 1 nitamkatilia mbali kila mtenda mabaya 2 kutoka mji wa Bwana.