Psalms 57
1Unihurumie, Ee Mungu, unihurumie, 2 kwa maana nafsi yangu inakukimbilia. 1 Chini ya uvuli wa mbawa zako nitakimbilia 2 mpaka maafa yapite. 1
2Namlilia Mungu Aliye Juu Sana, 2 Mungu atimizaye makusudi yake kwangu. 1
3Hutumana kutoka mbinguni na kuniokoa, 2 akiwakemea wale wanaonifuatilia vikali; 2 Mungu huutuma upendo wake na uaminifu wake. 1
4Niko katikati ya simba, 2 nimelala katikati ya wanyama wenye njaa kuu: 2 watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, 2 ambao ndimi zao ni panga kali. 1
5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, 2 utukufu wako na uenee duniani kote. 1
6Waliitegea miguu yangu nyavu, 2 nikainamishwa chini na dhiki. 1 Wamechimba shimo katika njia yangu, 2 lakini wametumbukia humo wao wenyewe. 1
7Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; 2 nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote. 1
8Amka, nafsi yangu! 2 Amka, kinubi na zeze! 2 Nitayaamsha mapambazuko. 1
9Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; 2 nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu. 1
10Kwa maana upendo wako ni mkuu, waenea hadi mbinguni, 2 uaminifu wako unazifikia anga. 1
11Ee Mungu, utukuzwe juu mbinguni, 2 utukufu wako na uwe duniani pote.