Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 140

1Ee Bwana, niokoe, kutoka kwa watu waovu; 2 nilinde na watu wenye jeuri, 1

2ambao hupanga mipango mibaya mioyoni mwao, 2 na kuchochea vita siku zote. 1

3Wao hufanya ndimi zao kali kama za nyoka, 2 sumu ya nyoka iko midomoni mwao. 1

4Ee Bwana, niepushe na mikono ya waovu; 2 nilinde na watu wenye jeuri 2 wanaopanga kunikwaza miguu yangu. 1

5Wenye kiburi wameficha mtego wa kuninasa, 2 wametandaza kamba za wavu wao, 2 wametega mitego kwenye njia yangu. 1

6Ee Bwana, ninakuambia, “Wewe ni Mungu wangu.” 2 Ee Bwana, usikie kilio changu na kunihurumia. 1

7Ee Bwana Mwenyezi, Mwokozi wangu mwenye nguvu, 2 unikingaye kichwa changu siku ya vita: 1

8Ee Bwana, usiwape waovu matakwa yao, 2 usiache mipango yao ikafanikiwa, 2 wasije wakajisifu. 1

9Vichwa vya wanaonizunguka vifunikwe 2 na shida zinazosababishwa na midomo yao. 1

10Makaa ya mawe ya moto na yawaangukie! 2 Na watupwe motoni, 1 katika mashimo ya matope, 2 wasiinuke tena kamwe. 1

11Wasingiziaji wasifanikiwe katika nchi; 2 maafa na yawawinde watu wenye jeuri. 1

12Najua kwamba Bwana huwapatia maskini haki, 2 na kuitegemeza njia ya mhitaji. 1

13Hakika wenye haki watalisifu jina lako, 2 na waadilifu wataishi mbele zako.

← Psalms 139Read In The App, Free →Psalms 141 →

Study Psalms 140

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150