Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 62

1Kwa Mungu peke yake nafsi yangu inapata pumziko; 2 wokovu wangu watoka kwake. 1

2Yeye peke yake ndiye mwamba wangu na wokovu wangu; 1 yeye ni ngome yangu, sitatikisika kamwe. 1

3Mtamshambulia mtu hata lini? 2 Je, ninyi nyote mtamtupa chini, 2 ukuta huu ulioinama na uzio huu unaotikisika? 1

4Walikusudia kikamilifu kumwangusha 2 toka mahali pake pa fahari; 2 wanafurahia uongo. 1 Kwa vinywa vyao hubariki, 2 lakini ndani ya mioyo yao hulaani. 1

5Ee nafsi yangu, upumzike, kwa Mungu peke yake, 2 tumaini langu latoka kwake. 1

6Yeye peke yake ndiye mwamba wangu na wokovu wangu; 2 ndiye ngome yangu, sitatikisika. 1

7Wokovu wangu na heshima yangu viko kwa Mungu, 2 ndiye mwamba wangu wenye nguvu 2 na kimbilio langu. 1

8Enyi watu, mtumainini yeye wakati wote, 2 miminieni mioyo yenu kwake, 2 kwa kuwa Mungu ni kimbilio letu. 1

9Binadamu wa ngazi ya chini ni pumzi tu, 2 nao wa ngazi ya juu ni uongo tu; 1 wakipimwa kwenye mizani, si chochote; 2 wote kwa pamoja ni pumzi tu. 1

10Usitumainie vya udhalimu 2 wala usijivune kwa vitu vya wizi; 1 ingawa utajiri wako utaongezeka, 2 usiviwekee moyo wako. 1

11Jambo moja Mungu amelisema, 2 mambo mawili nimeyasikia: 1 kwamba, Ee Mungu, 2 wewe una nguvu, 1

12na kwamba, Ee Bwana, 2 wewe ni mwenye upendo. 1 Hakika utampa kila mtu thawabu 2 kwa kadiri ya alivyotenda.

← Psalms 61Read In The App, Free →Psalms 63 →

Study Psalms 62

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150