Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 60

1Ee Mungu, umetukataa na kutokea ghafula juu yetu, 2 umekasirika: sasa turejeshe upya! 1

2Umetetemesha nchi na kuipasua; 2 uiponye mavunjiko yake, kwa maana inatetemeka. 1

3Umewaonyesha watu wako nyakati za kukata tamaa; 2 umetunywesha mvinyo unaotuyumbisha. 1

4Kwa wale wanaokucha wewe, 2 umewainulia bendera, 2 ili iweze kutwekwa dhidi ya upinde. 1

5Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, 2 ili wale uwapendao wapate kuokolewa. 1

6Mungu amenena kutoka patakatifu pake: 2 “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi 2 na kulipima Bonde la Sukothi. 1

7Gileadi ni yangu na Manase ni yangu; 2 Efraimu ni kofia yangu ya chuma, 2 nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala. 1

8Moabu ni sinia langu la kunawia, 2 juu ya Edomu natupa kiatu changu; 2 nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.” 1

9Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? 2 Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu? 1

10Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, 2 na hutoki tena na majeshi yetu? 1

11Tuletee msaada dhidi ya adui, 2 kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu. 1

12Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, 2 naye atawaponda adui zetu.

← Psalms 59Read In The App, Free →Psalms 61 →

Study Psalms 60

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150