Psalms 143
1Ee Bwana, sikia sala yangu, 2 sikiliza kilio changu unihurumie; 1 katika uaminifu na haki yako 2 njoo unisaidie. 1
2Usimhukumu mtumishi wako, 2 kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako. 1
3Adui hunifuatilia, 2 hunipondaponda chini; 1 hunifanya niishi gizani 2 kama wale waliokufa zamani. 1
4Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, 2 moyo wangu ndani yangu unakata tamaa. 1
5Nakumbuka siku za zamani; 2 natafakari juu ya kazi zako zote, 1 naangalia juu ya kazi 2 ambazo mikono yako imezifanya. 1
6Nanyoosha mikono yangu kwako, 2 nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame. 1
7Ee Bwana, unijibu haraka, 2 roho yangu inazimia. 1 Usinifiche uso wako, 2 ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni. 1
8Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, 2 kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. 1 Nionyeshe njia nitakayoiendea, 2 kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu. 1
9Ee Bwana, uniokoe na adui zangu, 2 kwa kuwa nimejificha kwako. 1
10Nifundishe kufanya mapenzi yako, 2 kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, 1 Roho wako mwema na aniongoze 2 katika nchi tambarare. 1
11Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, 2 kwa haki yako nitoe katika taabu. 1
12Kwa upendo wako usiokoma, 2 nyamazisha adui zangu; 1 waangamize watesi wangu wote, 2 kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.