Psalms 89
1Nitaimba juu ya upendo mkuu wa Bwana milele; 2 kwa kinywa changu nitajulisha uaminifu wako 2 ujulikane kwa vizazi vyote. 1
2Nitatangaza kuwa upendo wako unasimama imara milele 2 na uaminifu wako umeuthibitisha mbinguni. 1
3Ulisema, “Nimefanya agano na mteule wangu, 2 nimemwapia mtumishi wangu Daudi, 1
4‘Nitaimarisha uzao wako milele 2 na kudumisha ufalme wako kwa vizazi vyote.’ ” 1
5Ee Bwana, mbingu zinayasifu maajabu yako, 2 uaminifu wako pia katika kusanyiko la watakatifu. 1
6Kwa kuwa ni nani katika mbingu 2 anayeweza kulinganishwa na Bwana? 1 Ni nani miongoni mwa viumbe vya mbinguni 2 aliye kama Bwana? 1
7Katika kusanyiko la watakatifu, Mungu huogopwa sana, 2 anahofiwa kuliko wote wanaomzunguka. 1
8Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, 2 ni nani aliye kama wewe? 1 Ee Bwana, wewe ni mwenye nguvu, 2 na uaminifu wako unakuzunguka. 1
9Wewe unatawala bahari yenye msukosuko; 2 wakati mawimbi yake yanapoinuka, wewe unayatuliza. 1
10Wewe ulimponda Rahabu + 89:10 Rahabu hapa ina maana jina la Misri kwa fumbo, yaani mwenye majivuno (lakini sio Rahabu wa Yos 2). 2 kama mmojawapo wa waliochinjwa; 1 kwa mkono wako wenye nguvu, 2 uliwatawanya adui zako. 1
11Mbingu ni zako, nayo nchi pia ni yako, 2 uliuwekea ulimwengu msingi 2 pamoja na vyote vilivyomo. 1
12Uliumba kaskazini na kusini; 2 Tabori na Hermoni wanaliimbia jina lako kwa furaha. 1
13Mkono wako umejaa uwezo; 2 mkono wako una nguvu, 2 mkono wako wa kuume umetukuzwa. 1
14Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako cha enzi; 2 upendo na uaminifu vinakutangulia. 1
15Heri ni wale ambao wamejifunza kukusifu kwa shangwe, 2 wanaotembea katika mwanga 2 wa uwepo wako, Ee Bwana. 1
16Wanashangilia katika jina lako mchana kutwa, 2 wanafurahi katika haki yako. 1
17Kwa kuwa wewe ni utukufu na nguvu yao, 2 kwa wema wako unatukuza pembe + 89:17 Pembe inawakilisha nguvu. yetu. 1
18Naam, ngao yetu ni mali ya Bwana, 2 na mfalme wetu mali ya Aliye Mtakatifu wa Israeli. 1
19Ulizungumza wakati fulani katika maono, 2 kwa watu wako waaminifu, ukasema: 1 “Nimeweka nguvu kwa shujaa, 2 nimemwinua kijana miongoni mwa watu. 1
20Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, 2 na nimemtia mafuta yangu matakatifu. 1
21Kitanga changu kitamtegemeza, 2 hakika mkono wangu utamtia nguvu. 1
22Hakuna adui atakayemtoza ushuru, 2 hakuna mtu mwovu atakayemwonea. 1
23Nitawaponda adui zake mbele zake 2 na kuwaangamiza watesi wake. 1
24Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, 2 kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa. 1
25Nitauweka mkono wake juu ya bahari, 2 mkono wake wa kuume juu ya mito. 1
26Naye ataniita kwa sauti, ‘Wewe ni Baba yangu, 2 Mungu wangu, Mwamba na Mwokozi wangu.’ 1
27Nitamteua pia awe mzaliwa wangu wa kwanza, 2 aliyetukuka kuliko wafalme wote wa dunia. 1
28Nitadumisha upendo wangu kwake milele, 2 na agano langu naye litakuwa imara. 1
29Nitaudumisha uzao wake milele, 2 kiti chake cha enzi kama mbingu zinavyodumu. 1
30“Kama wanae wataacha amri yangu 2 na wasifuate sheria zangu, 1
31kama wakihalifu maagizo yangu 2 na kutoshika amri zangu, 1
32nitaadhibu dhambi yao kwa fimbo, 2 uovu wao kwa kuwapiga, 1
33lakini sitauondoa upendo wangu kwake, 2 wala sitausaliti uaminifu wangu kamwe. 1
34Mimi sitavunja agano langu 2 wala sitabadili lile ambalo midomo yangu imelitamka. 1
35Mara moja na kwa milele, nimeapa kwa utakatifu wangu, 2 nami sitamdanganya Daudi: 1
36kwamba uzao wake utaendelea milele, 2 na kiti chake cha enzi kitadumu mbele zangu kama jua; 1
37kitaimarishwa milele kama mwezi, 2 shahidi mwaminifu angani.” 1
38Lakini wewe umemkataa, umemdharau, 2 umemkasirikia sana mpakwa mafuta wako. 1
39Umelikana agano lako na mtumishi wako, 2 na umeinajisi taji yake mavumbini. 1
40Umebomoa kuta zake zote, 2 na ngome zake zote umezifanya kuwa magofu. 1
41Wote wapitao karibu wamemnyangʼanya mali zake; 2 amekuwa dharau kwa jirani zake. 1
42Umeutukuza mkono wa kuume wa adui zake, 2 umewafanya watesi wake wote washangilie. 1
43Umegeuza makali ya upanga wake, 2 na hukumpa msaada katika vita. 1
44Umeikomesha fahari yake, 2 na kukiangusha kiti chake cha enzi. 1
45Umezifupisha siku za ujana wake, 2 umemfunika kwa vazi la aibu. 1
46Hata lini, Ee Bwana? Utajificha milele? 2 Ghadhabu yako itawaka kama moto hata lini? 1
47Kumbuka jinsi maisha yangu yanavyopita haraka. 2 Ni kwa ubatili kiasi gani umemuumba mwanadamu! 1
48Ni mtu gani awezaye kuishi na asione kifo, 2 au kujiokoa mwenyewe kutoka nguvu za kaburi? + 89:48 Kaburi hapa maana yake ni Kuzimu, kwa Kiebrania ni Sheol. 1
49Ee Bwana, uko wapi upendo wako mkuu wa mwanzoni, 2 ambao katika uaminifu wako ulimwapia Daudi? 1
50Bwana kumbuka jinsi mtumishi wako amesimangwa, 2 jinsi ninavyovumilia moyoni mwangu dhihaka za mataifa yote, 1
51dhihaka ambazo kwazo adui zako 2 wamenisimanga, Ee Bwana, 1 ambazo kwazo wamesimanga 2 kila hatua ya mpakwa mafuta wako. 1
52Msifuni Bwana milele! Amen na Amen.