Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 5

1Ee Bwana, tegea sikio maneno yangu, 2 uangalie kupiga kite kwangu. 1

2Sikiliza kilio changu ili unisaidie, 2 Mfalme wangu na Mungu wangu, 2 kwa maana kwako ninaomba. 1

3Asubuhi, unasikia sauti yangu, Ee Bwana; 2 asubuhi naleta haja zangu mbele zako, 2 na kusubiri kwa matumaini. 1

4Wewe si Mungu unayefurahia uovu, 2 kwako mtu mwovu hataishi. 1

5Wenye kiburi hawawezi kusimama mbele yako, 2 unawachukia wote watendao mabaya. 1

6Unawaangamiza wasemao uongo. 2 Bwana huwachukia 2 wamwagao damu na wadanganyifu. 1

7Lakini mimi, kwa rehema zako kuu, 2 nitakuja katika nyumba yako, 1 kwa unyenyekevu, nitasujudu 2 kuelekea Hekalu lako takatifu. 1

8Niongoze katika haki yako, Ee Bwana, 2 kwa sababu ya adui zangu, 2 nyoosha njia yako mbele yangu. 1

9Hakuna neno kinywani mwao linaloweza kuaminika, 2 mioyo yao imejaa maangamizi. 1 Koo lao ni kaburi lililo wazi, 2 kwa ndimi zao, wao hunena udanganyifu. 1

10Uwatangaze kuwa wenye hatia, Ee Mungu! 2 Hila zao ziwe anguko lao wenyewe. 1 Wafukuzie mbali kwa sababu ya dhambi zao nyingi, 2 kwa kuwa wamekuasi wewe. 1

11Lakini wote wakimbiliao kwako na wafurahi, 2 waimbe kwa shangwe daima. 1 Ueneze ulinzi wako juu yao, 2 ili wale wapendao jina lako 2 wapate kukushangilia. 1

12Kwa hakika, Ee Bwana, unawabariki wenye haki, 2 unawazunguka kwa wema wako kama ngao.

← Psalms 4Read In The App, Free →Psalms 6 →

Study Psalms 5

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150