Psalms 146
1Msifuni Bwana! + 146:1 Msifuni Bwana kwa Kiebrania ni Hallelu Yah. 1 Ee nafsi yangu, umsifu Bwana, 2
2Nitamsifu Bwana maisha yangu yote; 1 nitamwimbia Mungu wangu sifa 2 wakati wote niishipo. 1
3Usiweke tumaini lako kwa wakuu, 2 kwa wanadamu ambao hufa, 2 ambao hawawezi kuokoa. 1
4Roho yao itokapo hurudi mavumbini, 2 siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma. 1
5Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, 2 ambaye tumaini lake ni katika Bwana, Mungu wake, 1
6Muumba wa mbingu na nchi, 2 na bahari na vyote vilivyomo ndani yake: 1 Bwana anayedumu kuwa mwaminifu 2 milele na milele. 1
7Naye huwapatia haki walioonewa 2 na kuwapa wenye njaa chakula. 1 Bwana huwaweka wafungwa huru, 2
8Bwana huwafumbua vipofu macho, 1 Bwana huwainua waliolemewa na mizigo yao, 2 Bwana huwapenda wenye haki. 1
9Bwana huwalinda wageni 2 na kuwategemeza yatima na wajane, 2 lakini hupinga njia za waovu. 1
10Bwana atamiliki milele, 2 Mungu wako, ee Sayuni, 2 kwa vizazi vyote. 1 Msifuni Bwana.