Psalms 66
1Mpigieni Mungu kelele za shangwe, dunia yote! 2
2Imbeni utukufu wa jina lake; 2 mpeni sifa zake kwa utukufu! 1
3Mwambieni Mungu, “Jinsi gani yalivyo ya kutisha matendo yako! 2 Uwezo wako ni mkuu mno kiasi kwamba 2 adui wananyenyekea mbele zako. 1
4Dunia yote yakusujudia, 2 wanakuimbia wewe sifa, 2 wanaliimbia sifa jina lako.” 1
5Njooni mwone yale Mungu aliyoyatenda, 2 mambo ya kutisha aliyoyatenda 2 miongoni mwa wanadamu! 1
6Alifanya bahari kuwa nchi kavu, 2 wakapita kati ya maji kwa miguu, 2 njooni, tumshangilie. 1
7Yeye hutawala kwa uwezo wake milele, 2 macho yake huangalia mataifa yote: 2 waasi wasithubutu kujiinua dhidi yake. 1
8Enyi mataifa, msifuni Mungu wetu, 2 sauti ya sifa yake isikike, 1
9ameyahifadhi maisha yetu 2 na kuizuia miguu yetu kuteleza. 1
10Ee Mungu, wewe ulitujaribu, 2 ukatusafisha kama fedha. 1
11Umetuingiza kwenye nyavu 2 na umetubebesha mizigo mizito 2 migongoni mwetu. 1
12Uliwaruhusu watu watukalie vichwani, 2 tulipita kwenye moto na kwenye maji, 1 lakini ulituleta kwenye nchi 2 iliyojaa utajiri tele. 1
13Nitakuja hekaluni mwako na sadaka za kuteketezwa 2 na kukutimizia nadhiri zangu: 1
14nadhiri ambazo midomo yangu iliahidi 2 na nilizotamka kwa kinywa changu 2 nilipokuwa katika shida. 1
15Nitakutolea dhabihu za wanyama wanono 2 na sadaka za kondoo dume, 2 nitakutolea mafahali na mbuzi. 1
16Njooni msikilize ninyi nyote mnaomcha Mungu, 2 nami niwaambie aliyonitendea. 1
17Nilimlilia kwa kinywa changu, 2 sifa zake zilikuwa katika ulimi wangu. 1
18Kama ningekuwa nimeyaficha maovu moyoni mwangu, 2 Bwana asingekuwa amenisikiliza; 1
19lakini hakika Mungu amenisikiliza 2 na amesikia sauti yangu katika maombi. 1
20Sifa apewe Mungu, 2 ambaye hakulikataa ombi langu 2 wala kunizuilia upendo wake!