Psalms 118
1Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; 2 upendo wake wadumu milele. 1
2Israeli na aseme sasa: 2 “Upendo wake wadumu milele.” 1
3Nyumba ya Aroni na iseme sasa: 2 “Upendo wake wadumu milele.” 1
4Wote wamchao Bwana na waseme sasa: 2 “Upendo wake wadumu milele.” 1
5Wakati wa maumivu yangu makuu nilimlilia Bwana, 2 naye akanijibu kwa kuniweka huru. 1
6Bwana yuko pamoja nami, sitaogopa. 2 Mwanadamu anaweza kunitenda nini? 1
7Bwana yuko pamoja nami, 2 yeye ni msaidizi wangu. 1 Nitawatazama adui zangu 2 wakiwa wameshindwa. 1
8Ni bora kumkimbilia Bwana 2 kuliko kumtumainia mwanadamu. 1
9Ni bora kumkimbilia Bwana 2 kuliko kuwatumainia wakuu. 1
10Mataifa yote yalinizunguka, 2 lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. 1
11Walinizunguka pande zote, 2 lakini kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. 1
12Walinizunguka kama kundi la nyuki, 2 lakini walikufa haraka kama miiba iteketeayo; 2 kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali. 1
13Nilisukumwa nyuma karibu kuanguka, 2 lakini Bwana alinisaidia. 1
14Bwana ni nguvu yangu na wimbo wangu, 2 yeye amefanyika wokovu wangu. 1
15Sauti za shangwe na ushindi 2 zinavuma hemani mwa wenye haki: 1 “Mkono wa kuume wa Bwana 2 umetenda mambo makuu! 1
16Mkono wa kuume wa Bwana 2 umeinuliwa juu, 1 mkono wa kuume wa Bwana 2 umetenda mambo makuu!” 1
17Sitakufa, bali nitaishi, 2 nami nitatangaza yale Bwana aliyoyatenda. 1
18Bwana ameniadhibu vikali, 2 lakini hakuniacha nife. 1
19Nifungulie malango ya haki, 2 nami nitaingia na kumshukuru Bwana. 1
20Hili ni lango la Bwana 2 ambalo wenye haki wanaweza kuliingia. 1
21Nitakushukuru, kwa kuwa ulinijibu, 2 umekuwa wokovu wangu. 1
22Jiwe walilolikataa waashi, 2 limekuwa jiwe kuu la pembeni. 1
23Bwana ametenda hili, 2 nalo ni la kushangaza machoni petu. 1
24Hii ndiyo siku Bwana aliyoifanya, 2 tushangilie na kufurahi ndani yake. 1
25Ee Bwana, tuokoe, 2 Ee Bwana, utujalie mafanikio. 1
26Heri yule ajaye kwa jina la Bwana. 2 Kutoka nyumba ya Bwana tunakubariki. 1
27Bwana ndiye Mungu, 2 naye ametuangazia nuru yake. 1 Mkiwa na matawi mkononi, 2 unganeni kwenye maandamano ya sikukuu 2 hadi kwenye pembe za madhabahu. 1
28Wewe ni Mungu wangu, nitakushukuru, 2 wewe ni Mungu wangu, nitakutukuza. 1
29Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; 2 upendo wake wadumu milele.