Psalms 22
1Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha? 2 Kwa nini uko mbali hivyo kuniokoa? 2 Mbali hivyo na maneno ya kuugua kwangu? 1
2Ee Mungu wangu, ninalia mchana, lakini hunijibu, 2 hata usiku, sinyamazi. 1
3Hata hivyo umesimikwa katika kiti cha enzi kama Uliye Mtakatifu; 2 wewe ni sifa ya Israeli. + 22:3 Tafsiri zingine zinasema: uketiye juu ya sifa za Israeli. 1
4Kwako wewe baba zetu waliweka tumaini lao, 2 walikutumaini nawe ukawaokoa. 1
5Walikulilia wewe na ukawaokoa, 2 walikutegemea wewe nao hawakuaibika. 1
6Mimi ni mnyoo wala si mwanadamu, 2 wanaume wamenibeza, na watu wamenidharau. 1
7Wote wanionao hunidhihaki, 2 hunivurumishia matusi, wakitikisa vichwa vyao: 1
8Husema, “Anamtegemea Bwana, 2 basi Bwana na amwokoe. 1 Amkomboe basi, kwa maana 2 anapendezwa naye.” 1
9Hata hivyo ulinitoa tumboni, 2 ukanifanya nikutegemee, 1 hata nilipokuwa ninanyonya 2 matiti ya mama yangu. 1
10Nimekabidhiwa kwako tangu kuzaliwa, 2 toka tumboni mwa mama yangu 2 umekuwa Mungu wangu. 1
11Usiwe mbali nami, 2 kwa maana shida iko karibu 2 na hakuna wa kunisaidia. 1
12Mafahali wengi wamenizunguka, 2 mafahali wa Bashani wenye nguvu 2 wamenizingira. 1
13Simba wangurumao wanaorarua mawindo 2 yao hupanua vinywa vyao dhidi yangu. 1
14Nimemiminwa kama maji, 2 mifupa yangu yote imetoka katika viungo vyake. 1 Moyo wangu umegeuka kuwa nta, 2 umeyeyuka ndani yangu. 1
15Nguvu zangu zimekauka kama kigae, 2 ulimi wangu umegandamana 2 na kaakaa la kinywa changu, 1 kwa sababu umenilaza 2 katika mavumbi ya kifo. 1
16Mbwa wamenizunguka, 2 kundi la watu waovu limenizingira, 2 wametoboa mikono yangu na miguu yangu. 1
17Naweza kuhesabu mifupa yangu yote, 2 watu wananikodolea macho na kunisimanga. 1
18Wanagawana nguo zangu wao kwa wao, 2 na vazi langu wanalipigia kura. 1
19Lakini wewe, Ee Bwana, 2 usiwe mbali. 1 Ee Nguvu yangu, 2 uje haraka unisaidie. 1
20Okoa maisha yangu na upanga, 2 uhai wangu wa thamani kutoka nguvu za mbwa. 1
21Niokoe kutoka kinywani mwa simba, 2 niokoe kutoka pembe za mafahali mwitu. 1
22Nitalitangaza jina lako kwa ndugu zangu, 2 katika kusanyiko nitakusifu wewe. 1
23Ninyi ambao mnamcha Bwana, msifuni! 2 Ninyi nyote wazao wote wa Yakobo, mheshimuni yeye! 2 Mcheni yeye, ninyi wazao wote wa Israeli! 1
24Kwa maana hakupuuza wala kudharau 2 mateso ya aliyeonewa; 1 hakumficha uso wake 2 bali alisikiliza kilio chake ili amsaidie. 1
25Kwako wewe hutoka kiini cha sifa zangu katika kusanyiko kubwa, 2 nitatimiza nadhiri zangu mbele ya wale wakuchao wewe. 1
26Maskini watakula na kushiba, 2 wale wamtafutao Bwana watamsifu: 2 mioyo yenu na iishi milele! 1
27Miisho yote ya dunia itakumbuka 2 na kumgeukia Bwana, 1 nazo jamaa zote za mataifa 2 watasujudu mbele zake, 1
28kwa maana ufalme ni wa Bwana 2 naye hutawala juu ya mataifa. 1
29Matajiri wote wa dunia watasherehekea na kuabudu. 2 Wote waendao mavumbini 2 watapiga magoti mbele yake, 1 wote ambao hawawezi 2 kudumisha uhai wao. 1
30Wazao wa baadaye watamtumikia yeye; 2 vizazi vijavyo vitajulishwa habari za Bwana. 1
31Watatangaza haki yake kwa watu 2 ambao hawajazaliwa bado, 2 kwa maana yeye ametenda hili.