Psalms 51
1Ee Mungu, unihurumie, 2 kwa kadiri ya upendo wako usiokoma, 1 kwa kadiri ya huruma yako kuu, 2 uyafute makosa yangu. 1
2Unioshe na uovu wangu wote 2 na unitakase dhambi yangu. 1
3Kwa maana ninajua makosa yangu, 2 na dhambi yangu iko mbele yangu daima. 1
4Dhidi yako, wewe peke yako, nimetenda dhambi 2 na kufanya yaliyo mabaya machoni pako, 1 ili uthibitike kuwa wa kweli unenapo, 2 na kuwa na haki utoapo hukumu. 1
5Hakika mimi nilizaliwa mwenye dhambi, 2 mwenye dhambi tangu nilipotungwa mimba kwa mama yangu. 1
6Hakika wewe wapendezwa na kweli itokayo moyoni, 2 ndani sana ya moyo wangu wanifundisha hekima. 1
7Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi, 2 unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji. 1
8Unipe kusikia furaha na shangwe, 2 mifupa uliyoiponda na ifurahi. 1
9Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu, 2 na uufute uovu wangu wote. 1
10Ee Mungu, uniumbie moyo safi, 2 uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu. 1
11Usinitupe kutoka mbele zako 2 wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu. 1
12Unirudishie tena furaha ya wokovu wako, 2 unipe roho ya utii, ili initegemeze. 1
13Ndipo nitakapowafundisha wakosaji njia zako, 2 na wenye dhambi watakugeukia wewe. 1
14Ee Mungu, Mungu uniokoaye, 2 niokoe na hatia ya kumwaga damu, 2 nao ulimi wangu utaimba juu ya haki yako. 1
15Ee Bwana, fungua midomo yangu, 2 na kinywa changu kitatangaza sifa zako. 1
16Wewe hupendezwi na dhabihu, au ningaliileta, 2 hufurahii sadaka za kuteketezwa. 1
17Bali dhabihu za Mungu ni roho iliyovunjika, 2 moyo uliovunjika wenye toba, 2 Ee Mungu, hutaudharau. 1
18Kwa wema wa radhi yako uifanye Sayuni istawi, 2 ukazijenge upya kuta za Yerusalemu. 1
19Hapo ndipo kutakapokuwa na dhabihu za haki, 2 sadaka nzima za kuteketezwa za kukupendeza sana, 1 pia mafahali watatolewa 2 madhabahuni mwako.