Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 78

1Enyi watu wangu, sikieni mafundisho yangu, 2 sikilizeni maneno ya kinywa changu. 1

2Nitafungua kinywa changu kwa mafumbo, 2 nitazungumza mambo yaliyofichika, mambo ya kale: 1

3yale ambayo tuliyasikia na kuyajua, 2 yale ambayo baba zetu walituambia. 1

4Hatutayaficha kwa watoto wao; 2 tutakiambia kizazi kijacho 1 matendo yastahiliyo sifa ya Bwana, 2 uweza wake, na maajabu aliyoyafanya. 1

5Aliagiza amri kwa Yakobo 2 na akaweka sheria katika Israeli, 1 ambazo aliwaamuru baba zetu 2 wawafundishe watoto wao, 1

6ili kizazi kijacho kizijue, 2 pamoja na watoto ambao watazaliwa, 2 nao pia wapate kuwaeleza watoto wao. 1

7Ndipo wangeweka tumaini lao kwa Mungu, 2 nao wasingesahau matendo yake, 2 bali wangalizishika amri zake. 1

8Ili wasifanane na baba zao, 2 waliokuwa kizazi cha ukaidi na uasi, 1 ambao roho zao hazikuwa na uaminifu kwake, 2 ambao roho zao hazikumwamini. 1

9Watu wa Efraimu, ingawa walijifunga pinde, 2 walikimbia siku ya vita. 1

10Hawakulishika agano la Mungu 2 na walikataa kuishi kwa sheria yake. 1

11Walisahau aliyokuwa ameyatenda, 2 maajabu aliyokuwa amewaonyesha. 1

12Alitenda miujiza machoni mwa baba zao, 2 huko Soani, katika nchi ya Misri. 1

13Aliigawanya bahari akawapitisha, 2 alifanya maji yasimame imara kama ukuta. 1

14Aliwaongoza kwa wingu mchana 2 na kwa nuru kutoka kwenye moto usiku kucha. 1

15Alipasua miamba jangwani 2 na akawapa maji tele kama bahari, 1

16alitoa vijito kutoka kwenye jabali lililochongoka, 2 akayafanya maji yatiririke kama mito. 1

17Lakini waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, 2 wakiasi jangwani dhidi ya Aliye Juu Sana. 1

18Kwa makusudi walimjaribu Mungu, 2 wakidai vyakula walivyovitamani. 1

19Walinena dhidi ya Mungu, wakisema, 2 “Je, Mungu aweza kuandaa meza jangwani? 1

20Alipopiga mwamba, maji yalitoka kwa nguvu, 2 vijito vikatiririka maji mengi. 1 Lakini je, aweza kutupa chakula pia? 2 Je, anaweza kuwapa watu wake nyama?” 1

21Bwana alipowasikia, alikasirika sana, 2 moto wake ukawa dhidi ya Yakobo, 2 na ghadhabu yake ikawaka dhidi ya Israeli, 1

22kwa kuwa hawakumwamini Mungu, 2 wala kuutumainia ukombozi wake. 1

23Hata hivyo alitoa amri kwa anga zilizo juu 2 na kufungua milango ya mbingu, 1

24akawanyeshea mana ili watu wale; 2 aliwapa nafaka ya mbinguni. 1

25Watu walikula mkate wa malaika, 2 akawatumia chakula chote ambacho wangeliweza kula. 1

26Aliachia upepo wa mashariki kutoka kwenye mbingu 2 na kuuongoza upepo wa kusini kwa uwezo wake. 1

27Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, 2 ndege warukao kama mchanga wa pwani. 1

28Aliwafanya washuke ndani ya kambi yao, 2 kuzunguka mahema yao yote. 1

29Walikula na kusaza, 2 kwa maana alikuwa amewapa kile walichotamani. 1

30Kabla hawajamaliza kula walichokitamani, 2 hata kilipokuwa kingali bado vinywani mwao, 1

31hasira ya Mungu ikawaka juu yao, 2 akawaua wale waliokuwa na nguvu zaidi miongoni mwao, 2 akiwaangusha vijana wa Israeli. 1

32Licha ya haya yote, waliendelea kutenda dhambi, 2 licha ya maajabu yake, hawakuamini. 1

33Kwa hiyo akamaliza siku zao katika ubatili 2 na miaka yao katika vitisho. 1

34Kila mara Mungu alipowaua baadhi yao, 2 waliosalia walimtafuta, 2 walimgeukia tena kwa shauku. 1

35Walikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao, 2 kwamba Mungu Aliye Juu Sana alikuwa Mkombozi wao. 1

36Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, 2 wakisema uongo kwa ndimi zao, 1

37mioyo yao haikuwa thabiti kwake, 2 wala hawakuwa waaminifu katika agano lake. 1

38Hata hivyo alikuwa na huruma, 2 alisamehe maovu yao 2 na hakuwaangamiza. 1 Mara kwa mara alizuia hasira yake, 2 wala hakuchochea ghadhabu yake yote. 1

39Alikumbuka kwamba wao walikuwa nyama tu, 2 upepo upitao ambao haurudi. 1

40Mara ngapi walimwasi jangwani 2 na kumhuzunisha nyikani! 1

41Walimjaribu Mungu mara kwa mara, 2 wakamkasirisha yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli. 1

42Hawakukumbuka uwezo wake, 2 siku aliyowakomboa kutoka kwa mtesi, 1

43siku aliyoonyesha ishara zake za ajabu huko Misri, 2 maajabu yake huko Soani. 1

44Aligeuza mito yao kuwa damu, 2 hawakuweza kunywa maji kutoka vijito vyao. 1

45Aliwapelekea makundi ya mainzi yakawala, 2 na vyura wakawaharibu. 1

46Aliruhusu tunutu kuharibu mimea yao, 2 mazao yao kwa nzige. 1

47Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe 2 na mikuyu yao kwa mvua iliyochangamana na theluji. 1

48Aliwaachia mifugo yao mvua ya mawe, 2 akayapiga makundi ya wanyama wao kwa radi. 1

49Aliwafungulia hasira yake kali, 2 ghadhabu yake, hasira na uadui, 2 na kundi la malaika wa kuharibu. 1

50Aliitengenezea njia hasira yake, 2 hakuwaepusha na kifo, 2 bali aliwaachia tauni. 1

51Aliwapiga wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, 2 matunda ya kwanza ya ujana katika mahema ya Hamu. 1

52Lakini aliwatoa watu wake kama kundi, 2 akawaongoza kama kondoo kupitia jangwani. 1

53Aliwaongoza salama, wala hawakuogopa, 2 bali bahari iliwameza adui zao. 1

54Hivyo akawaleta hadi kwenye mpaka wa nchi yake takatifu, 2 hadi nchi ya vilima ambayo mkono wake wa kuume ulikuwa umeitwaa. 1

55Aliyafukuza mataifa mbele yao, 2 na kuwagawia nchi zao kama urithi, 2 aliwakalisha makabila ya Israeli katika makao yao. 1

56Lakini wao walimjaribu Mungu, 2 na kuasi dhidi ya Yeye Aliye Juu Sana, 2 wala hawakuzishika sheria zake. 1

57Kama baba zao, hawakuwa thabiti wala waaminifu, 2 wakawa wasioweza kutegemewa 2 kama upinde wenye kasoro. 1

58Wakamkasirisha Mungu kwa mahali pao pa juu pa kuabudia miungu, 2 wakachochea wivu wake kwa sanamu zao. 1

59Wakati Mungu alipowasikia, alikasirika sana, 2 akamkataa Israeli kabisa. 1

60Akaiacha hema ya Shilo, 2 hema aliyokuwa ameiweka katikati ya wanadamu. 1

61Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, 2 utukufu wake mikononi mwa adui. 1

62Aliachia watu wake wauawe kwa upanga, 2 akaukasirikia sana urithi wake. 1

63Moto uliwaangamiza vijana wao, 2 na wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi, 1

64makuhani wao waliuawa kwa upanga, 2 wala wajane wao hawakuweza kulia. 1

65Ndipo Bwana alipoamka kama vile kuamka usingizini, 2 kama vile mtu aamkavyo kutoka kwenye bumbuazi la mvinyo. 1

66Aliwapiga na kuwashinda adui zake, 2 akawatia katika aibu ya milele. 1

67Ndipo alipozikataa hema za Yosefu, 2 hakulichagua kabila la Efraimu, 1

68lakini alilichagua kabila la Yuda, 2 Mlima Sayuni, ambao aliupenda. 1

69Alijenga patakatifu pake kama vilele, 2 kama dunia ambayo aliimarisha milele. 1

70Akamchagua Daudi mtumishi wake 2 na kumtoa kwenye mazizi ya kondoo. 1

71Kutoka kuchunga kondoo alimleta 2 kuwa mchungaji wa watu wake Yakobo, 2 wa Israeli urithi wake. 1

72Naye Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo, 2 kwa mikono ya ustadi aliwaongoza.

← Psalms 77Read In The App, Free →Psalms 79 →

Study Psalms 78

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150