Psalms 132
1Ee Bwana, mkumbuke Daudi 2 na taabu zote alizozistahimili. 1
2Aliapa kiapo kwa Bwana 2 na akaweka nadhiri kwa Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo: 1
3“Sitaingia nyumbani mwangu 2 au kwenda kitandani mwangu: 1
4sitaruhusu usingizi katika macho yangu, 2 wala kope zangu kusinzia, 1
5mpaka nitakapompatia Bwana mahali, 2 makao kwa ajili ya Yule Mwenye Nguvu wa Yakobo.” 1
6Tulisikia habari hii huko Efrathi, 2 tulikutana nayo katika mashamba ya Yaara: + 132:6 Yaani Kiriath-Yearimu. 1
7“Twendeni kwenye makao yake, 2 na tuabudu kwenye kiti cha kuwekea miguu yake; 1
8inuka, Ee Bwana, uje mahali pako pa kupumzikia, 2 wewe na Sanduku la nguvu zako. 1
9Makuhani wako na wavikwe haki, 2 watakatifu wako na waimbe kwa furaha.” 1
10Kwa ajili ya Daudi mtumishi wako, 2 usimkatae mpakwa mafuta wako. 1
11Bwana alimwapia Daudi kiapo, 2 kiapo cha uhakika ambacho hatakitangua: 1 “Nitamweka mmoja wa wazao wako mwenyewe 2 katika kiti chako cha enzi, 1
12kama wanao watashika Agano langu 2 na sheria ninazowafundisha, 1 ndipo wana wao watarithi 2 kiti chako cha enzi milele na milele.” 1
13Kwa maana Bwana ameichagua Sayuni, 2 amepaonea shauku pawe maskani yake: 1
14“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele na milele; 2 hapa ndipo nitakapoketi nikitawala, kwa sababu nimepaonea shauku: 1
15Nitambariki kwa kumpa mahitaji tele: 2 nitashibisha maskini wake kwa chakula. 1
16Nitawavika makuhani wake wokovu, 2 nao watakatifu wake watadumu wakiimba kwa furaha. 1
17“Hapa nitamchipushia Daudi pembe, + 132:17 Pembe inawakilisha nguvu. 2 na kuweka taa kwa ajili ya masiya + 132:17 Masiya yaani mpakwa mafuta. wangu. 1
18Adui zake nitawavika aibu, 2 bali taji kichwani pake itangʼaa sana.”