Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 52

1Ewe jitu, mbona unajivunia ubaya? 2 Kwa nini unajivuna mchana kutwa, 2 wewe ambaye ni fedheha mbele za Mungu? 1

2Ulimi wako hupanga mashauri mabaya ya maangamizi. 2 Ni kama wembe mkali, ninyi mfanyao hila. 1

3Unapenda mabaya kuliko mema, 2 uongo kuliko kusema kweli. 1

4Unapenda kila neno lenye kudhuru, 2 ewe ulimi wenye hila! 1

5Hakika Mungu atakushusha chini 2 kwa maangamizi ya milele: 1 atakunyakua na kukuondoa kwa nguvu 2 kutoka hema yako, 2 atakungʼoa kutoka nchi ya walio hai. 1

6Wenye haki wataona na kuogopa, 2 watamcheka, wakisema, 1

7“Huyu ni yule mtu ambaye 2 hakumfanya Mungu kuwa ngome yake, 1 bali alitumainia wingi wa utajiri wake, 2 na akawa hodari kwa kuwaangamiza wengine!” 1 Neema Ya Mungu 1

8Lakini mimi ni kama mti wa mzeituni 2 unaostawi katika nyumba ya Mungu, 1 nautegemea upendo wa Mungu usiokoma 2 milele na milele. 1

9Nitakusifu milele kwa yale uliyoyatenda, 2 nitatumaini jina lako, kwa kuwa jina lako ni jema. 2 Nitakusifu mbele ya watakatifu wako.

← Psalms 51Read In The App, Free →Psalms 53 →

Study Psalms 52

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150