Psalms 79
1Ee Mungu, mataifa yameuvamia urithi wako, 2 wamelinajisi Hekalu lako takatifu, 2 wameifanya Yerusalemu kuwa magofu. 1
2Wametoa maiti za watumishi 2 kuwa chakula cha ndege wa angani 1 na nyama ya watakatifu wako 2 kwa wanyama wa nchi. 1
3Wamemwaga damu kama maji 2 kuzunguka Yerusalemu yote, 2 wala hakuna yeyote wa kuwazika. 1
4Tumekuwa kitu cha aibu kwa jirani zetu, 2 cha dharau na mzaha kwa wale wanaotuzunguka. 1
5Hata lini, Ee Bwana? Je, wewe utakasirika milele? 2 Wivu wako utawaka kama moto hadi lini? 1
6Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali, 2 juu ya falme za hao wasioliitia jina lako, 1
7kwa maana wamemrarua Yakobo 2 na kuharibu nchi ya makao yake. 1
8Usituhesabie dhambi za baba zetu, 2 huruma yako na itujie hima, 2 kwa maana tu wahitaji mno. 1
9Ee Mungu Mwokozi wetu, utusaidie, 2 kwa ajili ya utukufu wa jina lako; 1 tuokoe na kutusamehe dhambi zetu 2 kwa ajili ya jina lako. 1
10Kwa nini mataifa waseme, 2 “Yuko wapi Mungu wenu?” 1 Mbele ya macho yetu, 2 dhihirisha kati ya mataifa 1 kwamba unalipiza kisasi damu iliyomwagwa 2 ya watumishi wako. 1
11Kilio cha huzuni cha wafungwa kifike mbele zako; 2 kwa nguvu za mkono wako 2 hifadhi wale waliohukumiwa kufa. 1
12Walipize jirani zetu mara saba vifuani mwao 2 aibu walizovurumisha juu yako, Ee Bwana. 1
13Ndipo sisi watu wako, kondoo wa malisho yako, 2 tutakusifu milele; 1 toka kizazi hadi kizazi 2 tutasimulia sifa zako.