Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 44

1Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, 2 baba zetu wametueleza 1 yale uliyotenda katika siku zao, 2 siku za kale. 1

2Kwa mkono wako uliwafukuza mataifa 2 na ukawapanda baba zetu, 1 uliangamiza mataifa 2 na kuwastawisha baba zetu. 1

3Sio kwa upanga wao waliipata nchi, 2 wala si mkono wao uliwapatia ushindi; 1 ilikuwa ni kitanga cha mkono wako wa kuume, 2 na nuru ya uso wako, 2 kwa kuwa uliwapenda. 1

4Wewe ni mfalme wangu na Mungu wangu, 2 unayeamuru ushindi kwa Yakobo. 1

5Kwa uwezo wako tunawasukuma nyuma watesi wetu; 2 kwa jina lako tunawakanyaga adui zetu. 1

6Siutumaini upinde wangu, 2 upanga wangu hauniletei ushindi; 1

7bali wewe unatupa ushindi juu ya adui zetu, 2 unawaaibisha watesi wetu. 1

8Katika Mungu wetu tunajivuna mchana kutwa, 2 nasi tutalisifu jina lako milele. 1

9Lakini sasa umetukataa na kutudhili, 2 wala huendi tena na jeshi letu. 1

10Umetufanya turudi nyuma mbele ya adui, 2 nao watesi wetu wametuteka nyara. 1

11Umetuacha tutafunwe kama kondoo 2 na umetutawanya katika mataifa. 1

12Umewauza watu wako kwa fedha kidogo, 2 wala hukupata faida yoyote kwa mauzo yao. 1

13Umetufanya lawama kwa jirani zetu, 2 dharau na dhihaka kwa wale wanaotuzunguka. 1

14Umetufanya kuwa mithali miongoni mwa mataifa, 2 mataifa hutikisa vichwa vyao. 1

15Fedheha yangu iko mbele yangu mchana kutwa, 2 na uso wangu umejaa aibu tele, 1

16kwa ajili ya dhihaka ya wale wanaonilaumu na kunitukana, 2 kwa sababu ya adui, ambaye anatamani kulipiza kisasi. 1

17Hayo yote yametutokea, 2 ingawa tulikuwa hatujakusahau 2 wala hatujaenda kinyume na agano lako. 1

18Mioyo yetu ilikuwa haijarudi nyuma; 2 nyayo zetu zilikuwa hazijaiacha njia yako. 1

19Lakini ulituponda na kutufanya makao ya mbweha, 2 na ukatufunika kwa giza nene. 1

20Kama tungalikuwa tumelisahau jina la Mungu wetu 2 au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni, 1

21je, Mungu hangaligundua hili, 2 kwa kuwa anazijua siri za moyo? 1

22Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; 2 tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa. 1

23Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? 2 Zinduka! Usitukatae milele. 1

24Kwa nini unauficha uso wako 2 na kusahau taabu na mateso yetu? 1

25Tumeshushwa hadi mavumbini, 2 miili yetu imegandamana na ardhi. 1

26Inuka na utusaidie, 2 utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.

← Psalms 43Read In The App, Free →Psalms 45 →

Study Psalms 44

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150