Psalms 147
1Msifuni Bwana. 1 Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa, 2 jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye! 1
2Bwana hujenga Yerusalemu, 2 huwakusanya Israeli walio uhamishoni. 1
3Anawaponya waliovunjika mioyo 2 na kuvifunga vidonda vyao. 1
4Huzihesabu nyota 2 na huipa kila moja jina lake. 1
5Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, 2 ufahamu wake hauna kikomo. 1
6Bwana huwahifadhi wanyenyekevu 2 lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini. 1
7Mwimbieni Bwana kwa shukrani, 2 mpigieni Mungu wetu kinubi. 1
8Yeye huzifunika anga kwa mawingu, 2 huinyeshea ardhi mvua, 2 na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima. 1
9Huwapa chakula mifugo 2 na pia makinda ya kunguru yanapolia. 1
10Furaha yake haipo katika nguvu za farasi, 2 wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu. 1
11Bwana hupendezwa na wale wamchao, 2 wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma. 1
12Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu, 2 msifu Mungu wako, ee Sayuni, 1
13kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako 2 na huwabariki watu wako walio ndani yako. 1
14Huwapa amani mipakani mwenu 2 na kukushibisha kwa ngano safi kabisa. 1
15Hutuma amri yake duniani, 2 neno lake hukimbia kasi. 1
16Anatandaza theluji kama sufu 2 na kutawanya umande kama majivu. 1
17Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. 2 Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake? 1
18Hutuma neno lake na kuviyeyusha, 2 huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka. 1
19Amemfunulia Yakobo neno lake, 2 sheria zake na maagizo yake kwa Israeli. 1
20Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote, 2 hawazijui sheria zake. 1 Msifuni Bwana.