Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 109

1Ee Mungu, ambaye ninakusifu, 2 usiwe kimya, 1

2kwa maana watu waovu na wadanganyifu 2 wamefungua vinywa vyao dhidi yangu; 1 wasema dhidi yangu 2 kwa ndimi za udanganyifu. 1

3Wamenizunguka kwa maneno ya chuki, 2 wananishambulia bila sababu. 1

4Wanachonilipa badala ya urafiki wangu ni kunishtaki, 2 lakini mimi ninawaombea. 1

5Wananilipiza mabaya kwa mema, 2 chuki badala ya urafiki wangu. 1

6Agiza mtu mwovu ampinge, 2 mshtaki + 109:6 Mshtaki hapa maana yake ni Shetani. asimame mkono wake wa kuume. 1

7Anapohukumiwa, apatikane na hatia, 2 nayo maombi yake yamhukumu. 1

8Siku zake za kuishi na ziwe chache, 2 nafasi yake ya uongozi ichukuliwe na mtu mwingine. 1

9Watoto wake na waachwe yatima, 2 mke wake na awe mjane. 1

10Watoto wake na watangetange wakiomba, 2 na wafukuzwe kwenye magofu ya nyumba zao. 1

11Mtu anayemdai na ateke vyote alivyo navyo, 2 matunda ya kazi yake yatekwe nyara na wageni. 1

12Asiwepo mtu yeyote wa kumtendea mema 2 wala wa kuwahurumia yatima wake. 1

13Uzao wake na ukatiliwe mbali, 2 majina yao yafutike katika kizazi kifuatacho. 1

14Maovu ya baba zake na yakumbukwe 2 mbele za Bwana, 1 dhambi ya mama yake 2 isifutwe kamwe. 1

15Dhambi zao na zibaki daima mbele za Bwana, 2 ili apate kukatilia mbali kumbukumbu lao duniani. 1

16Kwa maana kamwe hakuweza kutenda wema, 2 bali alimfukuza mnyonge na mhitaji, 2 aliwafanyia jeuri wahitaji na waliovunjika moyo. 1

17Alipenda kulaani, 2 nayo laana ikampata; 1 hakupenda kubariki, 2 kwa hiyo baraka na ikae mbali naye. 1

18Alivaa kulaani kama vazi lake, 2 nayo laana ikamwingia mwilini mwake kama maji, 2 kwenye mifupa yake kama mafuta. 1

19Na iwe kama joho alilozungushiwa, 2 kama mshipi aliofungiwa daima. 1

20Haya na yawe malipo ya Bwana kwa washtaki wangu, 2 kwa wale wanaoninenea mabaya. 1

21Lakini wewe, Ee Bwana Mwenyezi, 2 unitendee wema kwa ajili ya jina lako, 2 uniokoe kwa wema wa pendo lako. 1

22Maana mimi ni maskini na mhitaji, 2 moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu. 1

23Ninafifia kama kivuli cha jioni, 2 nimerushwa-rushwa kama nzige. 1

24Magoti yangu yamelegea kwa kufunga, 2 mwili wangu umedhoofika na kukonda. 1

25Nimekuwa kitu cha kudharauliwa kwa washtaki wangu, 2 wanionapo, hutikisa vichwa vyao. 1

26Ee Bwana, Mungu wangu nisaidie, 2 niokoe sawasawa na upendo wako. 1

27Watu na wafahamu kuwa ni mkono wako, 2 kwamba wewe, Ee Bwana, umetenda hili. 1

28Wanaweza kulaani, lakini wewe utabariki, 2 watakaposhambulia wataaibishwa, 2 lakini mtumishi wako atashangilia. 1

29Washtaki wangu watavikwa fedheha, 2 na kufunikwa na aibu kama joho. 1

30Kwa kinywa changu nitamtukuza sana Bwana, 2 katika umati mkubwa nitamsifu. 1

31Kwa maana husimama mkono wa kuume wa mhitaji, 2 kuokoa maisha yake kutoka kwa wale wanaomhukumu.

← Psalms 108Read In The App, Free →Psalms 110 →

Study Psalms 109

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150