Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 107

1Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, 2 upendo wake wadumu milele. 1

2Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, 2 wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui, 1

3wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, 2 kutoka mashariki na magharibi, 2 kutoka kaskazini na kusini. 1

4Baadhi yao walitangatanga jangwani, 2 hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi. 1

5Walikuwa na njaa na kiu, 2 nafsi zao zikadhoofika. 1

6Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, 2 naye akawaokoa kutoka taabu yao. 1

7Akawaongoza kwa njia iliyo sawa 2 hadi mji ambao wangeweza kuishi. 1

8Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, 2 na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu, 1

9kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, 2 na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema. 1

10Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, 2 wafungwa wakiteseka katika minyororo, 1

11kwa sababu walikuwa wameasi 2 dhidi ya maneno ya Mungu 1 na kudharau shauri 2 la Aliye Juu Sana. 1

12Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; 2 walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia. 1

13Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, 2 naye akawaokoa kutoka taabu yao. 1

14Akawatoa katika giza na huzuni kuu 2 na akavunja minyororo yao. 1

15Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, 2 na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu, 1

16kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba 2 na kukata mapingo ya chuma. 1

17Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, 2 wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao. 1

18Wakachukia kabisa vyakula vyote, 2 wakakaribia malango ya mauti. 1

19Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, 2 naye akawaokoa kutoka taabu yao. 1

20Akalituma neno lake na kuwaponya, 2 akawaokoa kutoka maangamizo yao. 1

21Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, 2 na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu. 1

22Na watoe dhabihu za kushukuru, 2 na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha. 1

23Wengine walisafiri baharini kwa meli, 2 walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu. 1

24Waliziona kazi za Bwana, 2 matendo yake ya ajabu kilindini. 1

25Kwa maana alisema na kuamsha tufani 2 iliyoinua mawimbi juu. 1

26Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, 2 katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka. 1

27Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, 2 ujanja wao ukafikia ukomo. 1

28Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, 2 naye akawatoa kwenye taabu yao. 1

29Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, 2 mawimbi ya bahari yakatulia. 1

30Walifurahi ilipokuwa shwari, 2 naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani. 1

31Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, 2 na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu. 1

32Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, 2 na wamsifu katika baraza la wazee. 1

33Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, 2 chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu, 1

34nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, 2 kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo. 1

35Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, 2 nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo; 1

36aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, 2 nao wakajenga mji wangeweza kuishi. 1

37Walilima mashamba na kupanda mizabibu, 2 nayo ikazaa matunda mengi, 1

38Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, 2 wala hakuruhusu mifugo yao kupungua. 1

39Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa 2 kwa kuonewa, maafa na huzuni. 1

40Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, 2 aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia. 1

41Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, 2 na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo. 1

42Wanyofu wataona na kufurahi, 2 lakini waovu wote watafunga vinywa vyao. 1

43Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, 2 na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

← Psalms 106Read In The App, Free →Psalms 108 →

Study Psalms 107

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150