Psalms 108
1Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; 2 nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote. 1
2Amka, kinubi na zeze! 2 Nitayaamsha mapambazuko. 1
3Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; 2 nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu. 1
4Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; 2 uaminifu wako unazifikia anga. 1
5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, 2 utukufu wako na uenee duniani kote. 1
6Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, 2 ili wale uwapendao wapate kuokolewa. 1
7Mungu amenena kutoka patakatifu pake: 2 “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi 2 na kulipima Bonde la Sukothi. 1
8Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, 2 Efraimu ni kofia yangu ya chuma, 2 nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala. 1
9Moabu ni sinia langu la kunawia, 2 juu ya Edomu natupa kiatu changu; 2 nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.” 1
10Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? 2 Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu? 1
11Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, 2 na hutoki tena na majeshi yetu? 1
12Tuletee msaada dhidi ya adui, 2 kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu. 1
13Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, 2 naye atawaponda adui zetu.