Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 106

1Msifuni Bwana. 1 Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; 2 upendo wake wadumu milele. 1

2Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana 2 au kutangaza kikamilifu sifa zake? 1

3Heri wale wanaodumisha haki, 2 ambao daima wanafanya yaliyo mema. 1

4Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, 2 uwe msaada wangu unapowaokoa, 1

5ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, 2 niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, 2 na kuungana na urithi wako katika kukusifu. 1

6Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, 2 tumekosa na tumetenda uovu. 1

7Wakati baba zetu walipokuwa Misri, 2 hawakuzingatia maajabu yako, 1 wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, 2 bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu. 1

8Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, 2 ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu. 1

9Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, 2 akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani. 1

10Aliwaokoa mikononi mwa adui; 2 kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa. 1

11Maji yaliwafunika adui zao, 2 hakunusurika hata mmoja. 1

12Ndipo walipoamini ahadi zake, 2 nao wakaimba sifa zake. 1

13Lakini mara walisahau aliyowatendea, 2 wala hawakungojea shauri lake. 1

14Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, 2 walimjaribu Mungu nyikani. 1

15Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, 2 lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha. 1

16Kambini walimwonea wivu Mose, 2 na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana. 1

17Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, 2 ikawazika Abiramu na kundi lake. 1

18Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, 2 mwali wa moto uliwateketeza waovu. 1

19Huko Horebu walitengeneza ndama, 2 na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma. 1

20Waliubadilisha Utukufu wao 2 kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani. 1

21Walimsahau Mungu aliyewaokoa, 2 aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri, 1

22miujiza katika nchi ya Hamu 2 na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu. 1

23Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: 2 kama Mose mteule wake, 1 asingesimama kati yao na Mungu 2 kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza. 1

24Kisha waliidharau ile nchi nzuri, 2 hawakuiamini ahadi yake. 1

25Walinungʼunika ndani ya mahema yao, 2 wala hawakumtii Bwana. 1

26Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa 2 kwamba atawafanya waanguke jangwani, 1

27kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, 2 na kuwatawanya katika nchi zote. 1

28Walijifunga nira na Baali wa Peori, 2 wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai. 1

29Waliichochea hasira ya Bwana, 2 wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, 2 nayo tauni ikazuka katikati yao. 1

30Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, 2 nayo tauni ikazuiliwa. 1

31Hili likahesabiwa kwake haki, 2 kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo. 1

32Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, 2 janga likampata Mose kwa sababu yao; 1

33kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, 2 na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose. 1

34Hawakuyaangamiza yale mataifa 2 kama Bwana alivyowaagiza, 1

35bali walijichanganya na mataifa 2 na wakazikubali desturi zao. 1

36Waliabudu sanamu zao, 2 zikawa mtego kwao. 1

37Wakawatoa wana wao 2 na binti zao dhabihu kwa mashetani. 1

38Walimwaga damu isiyo na hatia, 2 damu za wana wao na binti zao, 1 ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, 2 nayo nchi ikanajisika kwa damu zao. 1

39Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; 2 kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba. 1

40Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake 2 na akauchukia sana urithi wake. 1

41Akawakabidhi kwa mataifa 2 na adui zao wakawatawala. 1

42Adui zao wakawaonea 2 na kuwatia chini ya mamlaka yao. 1

43Mara nyingi aliwaokoa 2 lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, 2 nao wakajiharibu katika dhambi zao. 1

44Lakini akaangalia mateso yao 2 wakati aliposikia kilio chao; 1

45kwa ajili yao akakumbuka agano lake, 2 na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake. 1

46Akawafanya wahurumiwe 2 na wote waliowashikilia mateka. 1

47Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. 2 Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, 1 ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, 2 na kushangilia katika sifa zako. 1

48Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, 2 tangu milele na hata milele. 1 Watu wote na waseme, “Amen!” 1 Msifuni Bwana.

← Psalms 105Read In The App, Free →Psalms 107 →

Study Psalms 106

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150