Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 37

1Usisumbuke kwa ajili ya watendao maovu, 2 wala usiwaonee wivu watendao mabaya, 1

2kwa maana kama majani watanyauka mara, 2 kama mimea ya kijani watakufa mara. 1

3Mtumaini Bwana na utende yaliyo mema; 2 Kaa katika nchi ukafurahie malisho salama. 1

4Jifurahishe katika Bwana 2 naye atakupa haja za moyo wako. 1

5Mkabidhi Bwana njia yako, 2 mtumaini yeye, naye atatenda hili: 1

6Yeye atafanya haki yako ingʼae kama mapambazuko, 2 na hukumu ya shauri lako kama jua la adhuhuri. 1

7Tulia mbele za Bwana 2 na umngojee kwa uvumilivu; 1 usisumbuke watu wanapofanikiwa katika njia zao, 2 wanapotekeleza mipango yao miovu. 1

8Epuka hasira na uache ghadhabu, 2 usihangaike: itakuongoza tu kutenda uovu. 1

9Kwa maana waovu watakatiliwa mbali, 2 bali wale wanaomtumaini Bwana watairithi nchi. 1

10Bado kitambo kidogo, nao waovu hawataonekana, 2 ingawa utawatafuta, hawataonekana. 1

11Bali wanyenyekevu watairithi nchi 2 na wafurahie amani tele. 1

12Waovu hula njama dhidi ya wenye haki 2 na kuwasagia meno, 1

13bali Bwana huwacheka waovu, 2 kwa sababu anajua siku yao inakuja. 1

14Waovu huchomoa upanga 2 na kupinda upinde, 1 ili wawaangushe maskini na wahitaji, 2 kuwachinja wale ambao njia zao ni nyofu. 1

15Lakini panga zao zitachoma mioyo yao wenyewe, 2 na pinde zao zitavunjwa. 1

16Bora kidogo walicho nacho wenye haki 2 kuliko wingi wa mali wa waovu wengi; 1

17kwa maana nguvu za waovu zitavunjwa, 2 lakini Bwana humtegemeza mwenye haki. 1

18Bwana anazifahamu siku za wanyofu, 2 na urithi wao utadumu milele. 1

19Siku za maafa hawatanyauka, 2 siku za njaa watafurahia wingi wa vitu. 1

20Lakini waovu wataangamia: 2 Adui za Bwana watakuwa 2 kama uzuri wa mashamba, 1 watatoweka, 2 watatoweka kama moshi. 1

21Waovu hukopa na hawalipi, 2 bali wenye haki hutoa kwa ukarimu. 1

22Wale wanaobarikiwa na Bwana watairithi nchi, 2 bali wale anaowalaani watakatiliwa mbali. 1

23Kama Bwana akipendezwa na njia ya mtu, 2 yeye huimarisha hatua zake, 1

24ajapojikwaa, hataanguka, 2 kwa maana Bwana 2 humtegemeza kwa mkono wake. 1

25Nilikuwa kijana na sasa ni mzee, 2 lakini sijaona kamwe wenye haki wameachwa 2 au watoto wao wakiombaomba chakula. 1

26Wakati wote ni wakarimu na hukopesha bila masharti. 2 Watoto wao watabarikiwa. 1

27Acha ubaya na utende wema, 2 nawe utaishi katika nchi milele. 1

28Kwa kuwa Bwana huwapenda wenye haki 2 naye hatawaacha waaminifu wake. 1 Watalindwa milele, 2 lakini uzao wa waovu utakatiliwa mbali. 1

29Wenye haki watairithi nchi, 2 na kuishi humo milele. 1

30Kinywa cha mwenye haki hutamka hekima, 2 nao ulimi wake huzungumza lililo haki. 1

31Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; 2 nyayo zake hazitelezi. 1

32Watu waovu huvizia wenye haki, 2 wakitafuta kuwaua; 1

33lakini Bwana hatawaacha mikononi mwao 2 wala hatawaacha wahukumiwe 2 kuwa wakosa wanaposhtakiwa. 1

34Mngojee Bwana, 2 na uishike njia yake. 1 Naye atakutukuza uirithi nchi, 2 waovu watakapokatiliwa mbali, 2 utaliona hilo. 1

35Nimemwona mtu mwovu na mkatili akistawi 2 kama mwerezi wa Lebanoni, 1

36lakini alitoweka mara na hakuonekana, 2 ingawa nilimtafuta, hakupatikana. 1

37Watafakari watu wasio na hatia, 2 wachunguze watu wakamilifu, 2 kuna mafanikio kwa mtu apendaye amani. 1

38Lakini watenda dhambi wote wataangamizwa, 2 mafanikio yao yatakatiliwa mbali. 1

39Wokovu wa wenye haki hutoka kwa Bwana, 2 yeye ni ngome yao wakati wa shida. 1

40Bwana huwasaidia na kuwaokoa, 2 huwaokoa kutoka kwa waovu na kuwahifadhi, 2 kwa maana wanamkimbilia.

← Psalms 36Read In The App, Free →Psalms 38 →

Study Psalms 37

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150