Psalms 81
1Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; 2 mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo! 1
2Anzeni wimbo, pigeni matari, 2 pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri. 1
3Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume 2 wakati wa Mwandamo wa Mwezi, 1 na wakati wa mwezi mpevu, 2 katika siku ya Sikukuu yetu; 1
4hii ni amri kwa Israeli, 2 agizo la Mungu wa Yakobo. 1
5Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu 2 alipotoka dhidi ya Misri, 2 huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa. 1
6Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; 2 mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu. 1
7Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, 2 nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; 2 nilikujaribu katika maji ya Meriba. 1
8“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: 2 laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli! 1
9Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; 2 msimsujudie mungu wa kigeni. 1
10Mimi ni Bwana Mungu wako, 2 niliyekutoa nchi ya Misri. 1 Panua sana kinywa chako 2 nami nitakijaza. 1
11“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; 2 Israeli hakutaka kunitii. 1
12Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao 2 wafuate mashauri yao wenyewe. 1
13“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, 2 kama Israeli wangalifuata njia zangu, 1
14ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, 2 na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao! 1
15Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, 2 na adhabu yao ingedumu milele. 1
16Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, 2 na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”