Psalms 111
1Msifuni Bwana. 1 Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, 2 katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko. 1
2Kazi za Bwana ni kuu, 2 wote wanaopendezwa nazo huzitafakari. 1
3Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, 2 haki yake hudumu daima. 1
4Amefanya maajabu yake yakumbukwe, 2 Bwana ni mwenye neema na huruma. 1
5Huwapa chakula wale wanaomcha, 2 hulikumbuka agano lake milele. 1
6Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, 2 akiwapa nchi za mataifa mengine. 1
7Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, 2 mausia yake yote ni ya kuaminika. 1
8Zinadumu milele na milele, 2 zikifanyika kwa uaminifu na unyofu. 1
9Aliwapa watu wake ukombozi, 2 aliamuru agano lake milele: 2 jina lake ni takatifu na la kuogopwa. 1
10Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, 2 wote wanaozifuata amri zake wana busara. 2 Sifa zake zadumu milele.