Psalms 25
1Kwako wewe, Ee Bwana, 2 nainua nafsi yangu, 1
2ni wewe ninayekutumainia, 2 Ee Mungu wangu. 1 Usiniache niaibike, 2 wala usiache adui zangu wakanishinda. 1
3Kamwe hakuna hata mmoja anayekutegemea 2 atakayeaibishwa, 1 bali wataaibishwa 2 wafanyao hila bila sababu. 1
4Nionyeshe njia zako, Ee Bwana, 2 nifundishe mapito yako, 1
5niongoze katika kweli yako na kunifundisha, 2 kwa maana wewe ni Mungu Mwokozi wangu, 2 nalo tumaini langu liko kwako wakati wote. 1
6Kumbuka, Ee Bwana, rehema zako kuu na upendo, 2 kwa maana zimekuwepo tangu zamani. 1
7Usizikumbuke dhambi za ujana wangu 2 wala njia zangu za uasi, 1 sawasawa na upendo wako unikumbuke, 2 kwa maana wewe ni mwema, Ee Bwana. 1
8Bwana ni mwema na mwenye adili, 2 kwa hiyo huwafundisha wenye dhambi njia zake. 1
9Huwaongoza wanyenyekevu katika haki, 2 naye huwafundisha njia yake. 1
10Njia zote za Bwana ni za upendo na uaminifu 2 kwa wale wanaoshika shuhuda za agano lake. 1
11Ee Bwana, kwa ajili ya jina lako, 2 unisamehe uovu wangu, ijapokuwa ni mwingi. 1
12Ni nani basi, mtu yule anayemcha Bwana? 2 Atamfundisha katika njia 2 atakayoichagua kwa ajili yake. 1
13Mtu huyo atafanikiwa maishani mwake, 2 nao wazao wake watairithi nchi. 1
14Siri ya Bwana iko kwa wale wamchao, 2 yeye huwajulisha agano lake. 1
15Macho yangu humwelekea Bwana daima, 2 kwa kuwa yeye peke yake ndiye ataitoa 2 miguu yangu kutoka mtego. 1
16Nigeukie na unihurumie, 2 kwa maana mimi ni mpweke na mwenye kuteseka. 1
17Shida za moyo wangu zimeongezeka, 2 niokoe katika dhiki yangu. 1
18Uangalie mateso na shida zangu 2 na uniondolee dhambi zangu zote. 1
19Tazama adui zangu walivyo wengi, 2 pia uone jinsi wanavyonichukia vikali! 1
20Uyalinde maisha yangu na uniokoe, 2 usiniache niaibike, 2 kwa maana nimekukimbilia wewe. 1
21Uadilifu na uaminifu vinilinde, 2 kwa sababu tumaini langu ni kwako. 1
22Ee Mungu, wakomboe Israeli, 2 katika shida zao zote!