Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 145

1Nitakutukuza wewe, Mungu wangu Mfalme, 2 nitalisifu jina lako milele na milele. 1

2Kila siku nitakusifu 2 na kulitukuza jina lako milele na milele. 1

3Bwana ni mkuu, anayestahili kusifiwa sana, 2 ukuu wake haupimiki. 1

4Kizazi kimoja kitasifia kazi zako kwa kizazi kingine, 2 watasimulia matendo yako makuu. 1

5Watasema juu ya utukufu wa fahari ya ukuu wako, 2 nami nitatafakari juu ya kazi zako za ajabu. 1

6Watasimulia uwezo wa kazi zako za kutisha, 2 nami nitatangaza matendo yako makuu. 1

7Wataadhimisha wema wako mwingi, 2 na wataimba kwa shangwe juu ya haki yako. 1

8Bwana ni mwenye neema na mwingi wa huruma, 2 si mwepesi wa hasira, bali ni mwingi wa upendo. 1

9Bwana ni mwema kwa wote, 2 ana huruma kwa vyote alivyovifanya. 1

10Ee Bwana, vyote ulivyovifanya vitakusifu, 2 watakatifu wako watakutukuza. 1

11Watasimulia utukufu wa ufalme wako 2 na kusema juu ya ukuu wako, 1

12ili watu wote wajue matendo yako makuu 2 na utukufu wa fahari ya ufalme wako. 1

13Ufalme wako ni ufalme wa milele, 2 mamlaka yako hudumu vizazi vyote. 1 Bwana ni mwaminifu kwa ahadi zake zote 2 na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya. 1

14Bwana huwategemeza wote waangukao, 2 na huwainua wote waliolemewa na mizigo yao. 1

15Macho yao wote yanakutazama wewe, 2 nawe huwapa chakula chao wakati wake. 1

16Waufumbua mkono wako, 2 watosheleza haja ya kila kitu kilicho hai. 1

17Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, 2 na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya. 1

18Bwana yu karibu na wote wamwitao, 2 karibu na wote wamwitao kwa uaminifu. 1

19Huwatimizia wamchao matakwa yao, 2 husikia kilio chao na kuwaokoa. 1

20Bwana huwalinda wote wampendao, 2 bali waovu wote atawaangamiza. 1

21Kinywa changu kitazinena sifa za Bwana. 2 Kila kiumbe na kilisifu jina lake takatifu 2 milele na milele.

← Psalms 144Read In The App, Free →Psalms 146 →

Study Psalms 145

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150