Psalms 144
1Sifa ni kwa Bwana Mwamba wangu, 2 aifundishaye mikono yangu vita, 2 na vidole vyangu kupigana. 1
2Yeye ni Mungu wangu wa upendo na boma langu, 2 ngome yangu na mwokozi wangu, 1 ngao yangu ninayemkimbilia, 2 ambaye huwatiisha mataifa chini yangu. 1
3Ee Bwana, mwanadamu ni nini hata umjali, 2 Binadamu ni nini hata umfikirie? 1
4Mwanadamu ni kama pumzi, 2 siku zake ni kama kivuli kinachopita. 1
5Ee Bwana, pasua mbingu zako, ushuke, 2 gusa milima ili itoe moshi. 1
6Peleka umeme uwatawanye adui, 2 lenga mishale yako uwashinde. 1
7Nyoosha mkono wako kutoka juu, 2 nikomboe na kuniokoa 1 kutoka maji makuu, 2 kutoka mikononi mwa wageni 1
8ambao vinywa vyao vimejaa uongo, 2 na mikono yao ya kuume ni midanganyifu. 1
9Ee Mungu, nitakuimbia wimbo mpya, 2 kwa zeze yenye nyuzi kumi nitakuimbia, 1
10kwa Yule awapaye wafalme ushindi, 2 ambaye humwokoa Daudi, mtumishi wake kutokana na upanga hatari. 1
11Nikomboe na uniokoe 2 kutoka mikononi mwa wageni 1 ambao vinywa vyao vimejaa uongo, 2 na mikono yao ya kuume ni midanganyifu. 1
12Kisha wana wetu wakati wa ujana wao 2 watakuwa kama mimea iliyotunzwa vizuri, 1 binti zetu watakuwa kama nguzo zilizoviringwa 2 kurembesha jumba la kifalme. 1
13Ghala zetu zitajazwa 2 aina zote za mahitaji. 1 Kondoo zetu watazaa kwa maelfu, 2 kwa makumi ya maelfu katika mashamba yetu; 1
14maksai wetu watakokota 2 mizigo mizito. 1 Hakutakuwa na kubomoka kuta, 2 hakuna kuchukuliwa mateka, 1 wala kilio cha taabu 2 katika barabara zetu. 1
15Heri watu ambao hili ni kweli; 2 heri wale ambao Bwana ni Mungu wao.