Psalms 56
1Ee Mungu unihurumie, maana watu wananifuatia vikali; 2 mchana kutwa wanazidisha mashambulizi yao. 1
2Wasingiziaji wangu wananifuatia mchana kutwa, 2 wengi wananishambulia kwa kiburi chao. 1
3Wakati ninapoogopa, 2 nitakutumaini wewe. 1
4Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, 2 katika Mungu ninatumaini; sitaogopa. 1 Mwanadamu apatikanaye na kufa, 2 atanitenda nini? 1
5Mchana kutwa wanayageuza maneno yangu, 2 siku zote wanapanga shauri la kunidhuru. 1
6Wananifanyia hila, wanajificha, 2 wanatazama hatua zangu, 2 wakiwa na shauku ya kuutoa uhai wangu. 1
7Wasiepuke kwa vyovyote, 2 Ee Mungu, katika hasira yako yaangushe mataifa. 1
8Andika maombolezo yangu, 2 orodhesha machozi yangu katika gombo lako: 2 je, haya hayapo katika kumbukumbu zako? 1
9Ndipo adui zangu watarudi nyuma 2 ninapoita msaada. 1 Kwa hili nitajua kwamba Mungu 2 yuko upande wangu. 1
10Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu, 2 katika Bwana, ambaye neno lake ninalisifu, 1
11katika Mungu ninatumaini, sitaogopa. 2 Mwanadamu anaweza kunitenda nini? 1
12Ee Mungu, nina nadhiri kwako, 2 nitakutolea wewe sadaka zangu za shukrani. 1
13Kwa kuwa umeniokoa toka kwenye mauti 2 na miguu yangu kwenye kujikwaa, 1 ili niweze kuenenda mbele za Mungu 2 katika nuru ya uzima.