Psalms 77
1Nilimlilia Mungu ili anisaidie, 2 nilimlilia Mungu ili anisikie. 1
2Nilipokuwa katika taabu, nilimtafuta Bwana, 2 usiku nilinyoosha mikono bila kuchoka 2 na nafsi yangu ilikataa kufarijika. 1
3Ee Mungu, nilikukumbuka wewe, nikalia kwa huzuni; 2 nikatafakari, roho yangu ikadhoofika. 1
4Ulizuia macho yangu kufumba; 2 nilikuwa nasumbuka, nikashindwa kusema. 1
5Nilitafakari juu ya siku zilizopita, 2 miaka mingi iliyopita, 1
6nilikumbuka nilivyoimba nyimbo usiku. 2 Moyo wangu ulitafakari 2 na roho yangu ikauliza: 1
7“Je, Bwana atakataa milele? 2 Je, hatatenda mema tena? 1
8Je, upendo wake usio na mwisho umetoweka milele? 2 Je, ahadi yake imekoma nyakati zote? 1
9Je, Mungu amesahau kuwa na huruma? 2 Je, katika hasira amezuia huruma yake?” 1
10Ndipo nikawaza, “Huu ndio udhaifu wangu: 2 lakini nitakumbuka 1 miaka ya mkono wa kuume 2 wa Aliye Juu Sana.” 1
11Nitayakumbuka matendo ya Bwana; 2 naam, nitaikumbuka miujiza yako ya zamani. 1
12Nitazitafakari kazi zako zote 2 na kuyawaza matendo yako makuu. 1
13Ee Mungu, njia zako ni takatifu. 1 Ni mungu yupi aliye mkuu kama Mungu wetu? 1
14Wewe ndiwe Mungu utendaye miujiza, 2 umeonyesha uwezo wako katikati ya mataifa. 1
15Kwa mkono wako wenye nguvu umewakomboa watu wako, 2 uzao wa Yakobo na Yosefu. 1
16Maji yalikuona, Ee Mungu, 2 maji yalikuona yakakimbia, 2 vilindi vilitetemeka. 1
17Mawingu yalimwaga maji, 2 mbingu zikatoa ngurumo kwa radi, 2 mishale yako ikametameta huku na huko. 1
18Ngurumo yako ilisikika katika upepo wa kisulisuli, 2 umeme wako wa radi ukaangaza dunia, 2 nchi ikatetemeka na kutikisika. 1
19Njia yako ilipita baharini, 2 mapito yako kwenye maji makuu, 2 ingawa nyayo zako hazikuonekana. 1
20Uliongoza watu wako kama kundi 2 kwa mkono wa Mose na Aroni.