Psalms 137
1Kando ya mito ya Babeli tuliketi, tukaomboleza 2 tulipokumbuka Sayuni. 1
2Kwenye miti ya huko 2 tulitundika vinubi vyetu, 1
3kwa maana huko hao waliotuteka 2 walitaka tuwaimbie nyimbo, 1 watesi wetu walidai nyimbo za furaha; 2 walisema, “Tuimbieni wimbo mmoja kati ya nyimbo za Sayuni!” 1
4Tutaimbaje nyimbo za Bwana, 2 tukiwa nchi ya kigeni? 1
5Nikikusahau wewe, ee Yerusalemu, 2 basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake. 1
6Ulimi wangu ushikamane na kaakaa la kinywa changu 2 kama sitakukumbuka wewe, 1 kama nisipokufikiri Yerusalemu 2 kuwa furaha yangu kubwa. 1
7Kumbuka, Ee Bwana, walichokifanya Waedomu, 2 siku ile Yerusalemu ilipoanguka. 1 Walisema, “Bomoa, Bomoa 2 mpaka kwenye misingi yake!” 1
8Ee binti Babeli, uliyehukumiwa kuangamizwa, 2 heri yeye atakayekulipiza wewe 2 kwa yale uliyotutenda sisi: 1
9yeye ambaye atawakamata watoto wako wachanga 2 na kuwaponda juu ya miamba.