Psalms 141
1Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. 2 Sikia sauti yangu ninapokuita. 1
2Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; 2 kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni. 1
3Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, 2 weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu. 1
4Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, 2 nisije nikashiriki katika matendo maovu 1 pamoja na watu watendao mabaya, 2 wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa. 1
5Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; 2 na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. 2 Kichwa changu hakitalikataa. 1 Hata hivyo, maombi yangu daima 2 ni kinyume cha watenda mabaya, 1
6watawala wao watatupwa chini 2 kutoka kwenye majabali, 1 waovu watajifunza kwamba maneno yangu 2 yalikuwa kweli. 1
7Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, 2 ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” 1
8Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, 2 ndani yako nimekimbilia, usiniache nife. 1
9Niepushe na mitego waliyonitegea, 2 kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya. 1
10Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, 2 wakati mimi ninapita salama.