Psalms 46
1Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, 2 msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso. 1
2Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa 2 nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari. 1
3Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, 2 milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake. 1
4Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, 2 mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi. 1
5Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, 2 Mungu atausaidia asubuhi na mapema. 1
6Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, 2 Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka. 1
7Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, 2 Mungu wa Yakobo ni ngome yetu. 1
8Njooni mkaone kazi za Bwana 2 jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi. 1
9Anakomesha vita hata miisho ya dunia, 2 anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, 2 anateketeza ngao kwa moto. 1
10“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; 2 nitatukuzwa katikati ya mataifa, 2 nitatukuzwa katika dunia.” 1
11Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; 2 Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.