Psalms 80
1Ee Mchungaji wa Israeli tusikie, 2 wewe umwongozaye Yosefu kama kundi; 1 wewe uketiye katika kiti cha enzi 2 katikati ya makerubi, angaza 2
2mbele ya Efraimu, Benyamini na Manase. 1 Uamshe nguvu zako, 2 uje utuokoe. 1
3Ee Mungu, uturejeshe, 2 utuangazie uso wako, 2 ili tuweze kuokolewa. 1
4Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, 2 hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi 2 dhidi ya maombi ya watu wako? 1
5Umewalisha kwa mkate wa machozi, 2 umewafanya wanywe machozi bakuli tele. 1
6Tumekuwa chanzo cha ugomvi kwa jirani zetu, 2 na adui zetu wanatudhihaki. 1
7Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; 2 utuangazie uso wako, 2 nasi tuweze kuokolewa. 1
8Ulileta mzabibu kutoka Misri, 2 ukawafukuza mataifa, ukaupanda. 1
9Uliandaa shamba kwa ajili yake, 2 mizizi ikawa imara, ukajaza nchi. 1
10Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, 2 matawi yake yakafunika mierezi mikubwa. 1
11Matawi yake yalienea mpaka Baharini, + 80:11 Huenda inamaanisha Bahari ya Mediterania. 2 machipukizi yake mpaka kwenye Mto. + 80:11 Yaani Mto Frati. 1
12Mbona umebomoa kuta zake 2 ili wote wapitao karibu 2 wazichume zabibu zake? 1
13Nguruwe mwitu wanauharibu 2 na wanyama wa kondeni hujilisha humo. 1
14Turudie, Ee Mungu Mwenye Nguvu Zote! 2 Tazama chini kutoka mbinguni na uone! 1 Linda mzabibu huu, 2
15mche ulioupanda kwa mkono wako wa kuume, 1 mwana uliyemlea 2 kwa ajili yako mwenyewe. 1
16Mzabibu wako umekatwa, umechomwa moto, 2 unapowakemea, watu wako huangamia. 1
17Mkono wako na utulie juu ya mtu aliyeko mkono wako wa kuume, 2 mwana wa mtu uliyemlea kwa ajili yako mwenyewe. 1
18Ndipo hatutakuacha tena, 2 utuhuishe, nasi tutaliitia jina lako. 1
19Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, uturejeshe; 2 utuangazie uso wako, 2 ili tuweze kuokolewa.