Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 94

1Ee Bwana, ulipizaye kisasi, 2 Ee Mungu ulipizaye kisasi, uangaze sasa. 1

2Ee Mhukumu wa dunia, inuka, 2 uwalipize wenye kiburi kama wanavyostahili. 1

3Hata lini, waovu, Ee Bwana, 2 hata lini waovu watashangilia? 1

4Wanamimina maneno ya kiburi, 2 watenda mabaya wote wamejaa majivuno. 1

5Ee Bwana, wanawaponda watu wako, 2 wanawaonea urithi wako. 1

6Wanamchinja mjane na mgeni, 2 na kuwaua yatima. 1

7Nao husema, “ Bwana haoni, 2 Mungu wa Yakobo hafahamu.” 1

8Sikizeni, enyi wajinga miongoni mwa watu; 2 enyi wapumbavu, lini mtakuwa na hekima? 1

9Je, aliyeweka sikio asisikie? 2 Aliyeumba jicho asione? 1

10Je, anayeadhibisha mataifa asiadhibu? 2 Je, awafundishaye wanadamu asiwe na maarifa? 1

11Bwana anajua mawazo ya mwanadamu; 2 anajua kwamba ni ubatili. 1

12Ee Bwana, heri mtu anayeadhibishwa na wewe, 2 mtu unayemfundisha kwa sheria yako, 1

13unampa utulivu siku za shida, 2 mpaka shimo litakapokuwa limechimbwa 2 kwa ajili ya mwovu. 1

14Kwa kuwa Bwana hatawakataa watu wake, 2 hatauacha urithi wake. 1

15Hukumu itasimamishwa tena kwenye haki, 2 wote walio na mioyo minyofu wataifuata. 1

16Ni nani atakayeinuka dhidi ya mwovu kwa ajili yangu? 2 Ni nani atakayenikinga dhidi ya watenda maovu? 1

17Kama Bwana asingelinisaidia upesi, 2 ningelikuwa ninaishi katika ukimya wa kifo. 1

18Niliposema, “Mguu wangu unateleza,” 2 Ee Bwana, upendo wako ulinishikilia. 1

19Wakati wasiwasi ulipokuwa mwingi ndani yangu, 2 faraja yako ilinipa furaha nafsini mwangu. 1

20Je, kiti cha utawala wa udhalimu kitajiunga nawe, 2 ule utawala uletao taabu kutokana na sheria zake? 1

21Huungana kuwashambulia wenye haki, 2 kuwahukumu kufa wasio na hatia. 1

22Lakini Bwana amekuwa ngome yangu, 2 na Mungu wangu amekuwa mwamba ninaoukimbilia. 1

23Yeye atawalipa kwa ajili ya dhambi zao 2 na atawaangamiza kwa ajili ya maovu yao; 2 Bwana Mungu wetu atawaangamiza.

← Psalms 93Read In The App, Free →Psalms 95 →

Study Psalms 94

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150