Psalms 136
1Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema. Fadhili zake zadumu milele. 1
2Mshukuruni Mungu wa miungu. Fadhili zake zadumu milele. 1
3Mshukuruni Bwana wa mabwana: Fadhili zake zadumu milele. 1
4Kwake yeye pekee atendaye maajabu makuu, Fadhili zake zadumu milele. 1
5Ambaye kwa ufahamu wake aliziumba mbingu, Fadhili zake zadumu milele. 1
6Ambaye aliitandaza dunia juu ya maji, Fadhili zake zadumu milele. 1
7Ambaye aliumba mianga mikubwa, Fadhili zake zadumu milele. 1
8Jua litawale mchana, Fadhili zake zadumu milele. 1
9Mwezi na nyota vitawale usiku, Fadhili zake zadumu milele. 1
10Kwake yeye aliyemuua mzaliwa wa kwanza wa Misri, Fadhili zake zadumu milele. 1
11Na kuwatoa Israeli katikati yao, Fadhili zake zadumu milele. 1
12Kwa mkono wenye nguvu ulionyooshwa, Fadhili zake zadumu milele. 1
13Kwake yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, Fadhili zake zadumu milele. 1
14Na kuwapitisha Israeli katikati yake, Fadhili zake zadumu milele. 1
15Lakini alimfagia Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, Fadhili zake zadumu milele. 1
16Kwake yeye aliyewaongoza watu wake katika jangwa, Fadhili zake zadumu milele. 1
17Ambaye aliwapiga wafalme wenye nguvu, Fadhili zake zadumu milele. 1
18Naye aliwaua wafalme wenye nguvu, Fadhili zake zadumu milele. 1
19Sihoni mfalme wa Waamori, Fadhili zake zadumu milele. 1
20Ogu mfalme wa Bashani, Fadhili zake zadumu milele. 1
21Akatoa nchi yao kuwa urithi, Fadhili zake zadumu milele. 1
22Urithi kwa Israeli mtumishi wake, Fadhili zake zadumu milele. 1
23Aliyetukumbuka katika unyonge wetu, Fadhili zake zadumu milele. 1
24Alituweka huru toka adui zetu, Fadhili zake zadumu milele. 1
25Ambaye humpa chakula kila kiumbe. Fadhili zake zadumu milele. 1
26Mshukuruni Mungu wa mbinguni, Fadhili zake zadumu milele.