Psalms 9
1Ee Bwana, nitakutukuza kwa moyo wangu wote, 2 nitayasimulia matendo yako yote ya ajabu. 1
2Nitafurahi na kushangilia ndani yako. 2 Nitaliimbia sifa jina lako, Ewe Uliye Juu Sana. 1
3Adui zangu wamerudi nyuma, 2 wamejikwaa na kuangamia mbele zako. 1
4Kwa maana umetetea haki yangu na msimamo wangu; 2 umeketi kwenye kiti chako cha enzi, 2 ukihukumu kwa haki. 1
5Umekemea mataifa na kuwaangamiza waovu; 2 umeyafuta majina yao milele na milele. 1
6Uharibifu usiokoma umempata adui, 2 umeingʼoa miji yao; 2 hata kumbukumbu lao limetoweka. 1
7Bwana anatawala milele, 2 ameweka kiti chake cha enzi apate kuhukumu. 1
8Mungu atahukumu ulimwengu kwa haki, 2 atatawala mataifa kwa haki. 1
9Bwana ni kimbilio la watu wanaoonewa, 2 ni ngome imara wakati wa shida. 1
10Wote wanaolijua jina lako watakutumaini wewe, 2 kwa maana wewe Bwana, 2 hujawaacha kamwe wakutafutao. 1
11Mwimbieni Bwana sifa, amefanywa mtawala Sayuni, 2 tangazeni miongoni mwa mataifa, yale aliyoyatenda. 1
12Kwa maana yeye alipizaye kisasi cha damu hukumbuka, 2 hapuuzi kilio cha wanaoonewa. 1
13Ee Bwana, tazama jinsi walivyo wengi adui zangu wanaonitesa! 2 Nihurumie, uniinue kutoka malango ya mauti, 1
14ili niweze kutangaza sifa zako 2 katika malango ya Binti Sayuni 2 na huko niushangilie wokovu wako. 1
15Mataifa wameanguka kwenye shimo walilolichimba, 2 miguu yao imenaswa kwenye wavu waliouficha. 1
16Bwana anajulikana kwa haki yake, 2 waovu wamenaswa katika kazi za mikono yao. 1
17Waovu wataishia kuzimu, 2 naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu. 1
18Lakini mhitaji hatasahaulika siku zote, 2 wala matumaini ya walioonewa hayatapotea. 1
19Ee Bwana, inuka, usimwache binadamu ashinde. 2 Mataifa na yahukumiwe mbele zako. 1
20Ee Bwana, wapige kwa hofu, 2 mataifa na yajue kuwa wao ni watu tu.