Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 41

1Heri mtu yule anayemjali mnyonge, 2 Bwana atamwokoa wakati wa shida. 1

2Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, 2 atambariki katika nchi 2 na hatamwacha katika tamaa ya adui zake. 1

3Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, 2 atamwinua kutoka kitandani mwake. 1

4Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, 2 niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.” 1

5Adui zangu wanasema kwa hila, 2 “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.” 1

6Kila anapokuja mtu kunitazama, 2 huzungumza uongo, 1 huku moyo wake hukusanya masingizio; 2 kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko. 1

7Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, 2 hao huniwazia mabaya sana, wakisema, 1

8“Ugonjwa mbaya sana umempata, 2 kamwe hatainuka tena kitandani mwake.” 1

9Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, 2 yule aliyekula chakula changu 2 ameniinulia kisigino chake. 1

10Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, 2 ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi. 1

11Najua kwamba wapendezwa nami, 2 kwa kuwa adui yangu hanishindi. 1

12Katika uadilifu wangu unanitegemeza 2 na kuniweka kwenye uwepo wako milele. 1

13Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, 2 tangu milele na hata milele. Amen na Amen.

← Psalms 40Read In The App, Free →Psalms 42 →

Study Psalms 41

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150