Psalms 58
1Enyi watawala, je, kweli mwanena kwa haki? 2 Je, mnahukumu kwa unyofu miongoni mwa watu? 1
2La, mioyoni mwenu mnatunga udhalimu, 2 na mikono yenu hupima jeuri duniani. 1
3Waovu ni wapotovu tangu kuzaliwa kwao, 2 toka tumboni mwa mama zao 2 ni wakaidi na husema uongo. 1
4Sumu yao ni kama sumu ya nyoka, 2 kama ile ya fira ambaye ameziba masikio yake, 1
5ambaye hatasikia sauti ya kutumbuiza ya mwaguzi, 2 hata kama mganga angecheza kwa ustadi kiasi gani. 1
6Ee Mungu, yavunje meno katika vinywa vyao; 2 Ee Bwana, vunja meno makali ya hao simba! 1
7Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi, 2 wavutapo pinde zao, mishale yao na iwe butu. 1
8Kama konokono ayeyukavyo akitembea, 2 kama mtoto aliyezaliwa akiwa mfu, 2 wasilione jua. 1
9Kabla vyungu vyenu havijapata moto wa kuni za miiba, 2 zikiwa mbichi au kavu, 1 waovu watakuwa 2 wamefagiliwa mbali. 1
10Wenye haki watafurahi waonapo wakilipizwa kisasi, 2 watakapochovya nyayo zao katika damu ya waovu. 1
11Ndipo wanadamu watasema, 2 “Hakika utulivu wa wenye haki bado una thawabu, 2 hakika kuna Mungu ahukumuye dunia.”