Psalms · Biblia (Kiswahili)

Psalms 112

1Msifuni Bwana. 1 Heri mtu yule amchaye Bwana, 2 mtu yule apendezwaye sana na amri zake. 1

2Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, 2 kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa. 1

3Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, 2 haki yake hudumu milele. 1

4Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, 2 yule mwenye rehema, huruma na haki. 1

5Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, 2 anayefanya mambo yake kwa haki. 1

6Hakika hatatikisika kamwe, 2 mtu mwenye haki atakumbukwa milele. 1

7Hataogopa habari mbaya, 2 moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana. 1

8Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, 2 mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake. 1

9Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; 2 haki yake hudumu milele; 2 pembe yake itatukuzwa kwa heshima. 1

10Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, 2 atasaga meno yake na kutoweka, 2 kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

← Psalms 111Read In The App, Free →Psalms 113 →

Study Psalms 112

KJVMatthew HenryJamieson-Fausset-BrownAdam ClarkeJohn WesleyJohn CalvinKeil and DelitzschCharles SpurgeonScofieldFamily Bible NotesGeneva Bible Notes (1599)Reina-Valera (Español)Bíblia Almeida (Português)Luther Bibel (Deutsch)Bible Louis Segond (Français)

All Chapters

123456789101112131415161718192021222324252627282930313233343536373839404142434445464748495051525354555657585960616263646566676869707172737475767778798081828384858687888990919293949596979899100101102103104105106107108109110111112113114115116117118119120121122123124125126127128129130131132133134135136137138139140141142143144145146147148149150